Zaburi 144:1-15
Ya Daudi.
144 Yehova, Mwamba wangu,+ asifiwe,
Yeye mwenye kuzoeza mikono yangu kwa ajili ya pigano,
Vidole vyangu kwa ajili ya vita.+
2 Yeye ni upendo wangu mushikamanifu na ngome yangu,
Kimbilio langu salama* na mwokozi wangu,
Ngao yangu na Ule mwenye nimejificha ndani yake,+
Ule mwenye kutiisha vikundi vya watu chini yangu.+
3 Ee Yehova, mwanadamu ni nini ili umutambue,
Mwana wa mwanadamu mwenye anaweza kufa ni nini ili umukazie uangalifu?+
4 Mwanadamu anafanana na pumuzi tu;+
Siku zake ziko kama kivuli chenye kupita.+
5 Ee Yehova, shusha* mbingu zako na uteremuke;+
Gusa milima na uifanye itoe moshi.+
6 Fanya umeme wa radi uangaze na kusambaza maadui;+
Piga mishale yako na uwavuruge.+
7 Nyoosha mikono yako ukiwa juu;
Uniokoe na kunikomboa katika maji mengi,
Katika mukono wa* wageni,+
8 Wenye vinywa vyao vinasema uongo
Na wenye wanainua mukono wao wa kuume ili kuapa kwa uongo.*
9 Ee Mungu, nitakuimbia wimbo mupya.+
Nitakuimbia sifa,* kwa chombo cha kamba kumi (10),
10 Wewe mwenye kupatia wafalme ushindi,*+
Wewe mwenye kumuokoa mutumishi wako Daudi kutokana na upanga hatari.+
11 Uniokoe na kunikomboa katika mukono wa wageni,
Wenye vinywa vyao vinasema uongo
Na wenye wanainua mukono wao wa kuume ili kuapa kwa uongo.
12 Halafu watoto wetu wanaume watakuwa kama mimea michanga yenye kukomaa haraka,
Watoto wetu wanamuke kama nguzo za pembe zenye kuchongwa kwa ajili ya nyumba ya mufalme.
13 Madepo yetu yatajaa sana mazao ya kila namna;
Makundi yetu katika maeneo yetu ya mashamba yataongezeka kwa maelfu, kwa makumi ya maelfu.
14 Ngombe wetu, wakiwa na mimba, hawatapatwa na jambo la mubaya* wala mimba kuharibika,
Hakutakuwa kilio cha kuteseka katika viwanja vyetu vya watu wote.
15 Wenye furaha ni watu wenye kuwa katika hali hiyo!
Wenye furaha ni watu wenye Mungu wao ni Yehova!+
Maelezo ya Chini
^ Ao “Mahali pangu salama pa juu.”
^ Ao “kunja.”
^ Ao “kushikwa na.”
^ Tnn., “Na mukono wao wa kuume ni mukono wa kuume wa uongo.”
^ Ao “Nitakupigia muziki.”
^ Ao “wokovu.”
^ Ao “hawatapasukiwa na mimba.”