Zaburi 96:1-13
96 Mumuimbie Yehova wimbo mupya.+
Mumuimbie Yehova, dunia yote!+
2 Mumuimbie Yehova; musifu jina lake.
Mutangaze habari njema za wokovu wake siku kwa siku.+
3 Mutangaze utukufu wake kati ya mataifa,Kazi zake za ajabu kati ya vikundi vyote vya watu.+
4 Yehova ni mukubwa na anastahili kusifiwa sana.
Ni mwenye kuogopesha sana kuliko miungu mingine yote.
5 Miungu yote ya vikundi vya watu ni miungu yenye haina mafaa yoyote,+Lakini Yehova ndiye alifanya mbingu.+
6 Mbele yake kuko ukubwa* na utukufu;+Nguvu na uzuri viko katika patakatifu pake.+
7 Mumupatie Yehova kile chenye anastahili, ninyi familia za vikundi vya watu,Mumupatie Yehova kile chenye anastahili kwa sababu ya utukufu wake na nguvu zake.+
8 Mumupatie Yehova utukufu wenye jina lake linastahili;+Mulete zawadi na muingie katika viwanja vyake.
9 Mumuinamie* Yehova katika mapambo matakatifu;*Mutetemeke mbele yake, dunia yote!
10 Mutangaze kati ya mataifa: “Yehova amekuwa Mufalme!+
Dunia* imewekwa imara kabisa, haiwezi kuhamishwa.*
Atahukumu vikundi vya watu kwa haki.”*+
11 Mbingu zishangilie, na dunia ifurahi;Bahari ingurume na vyote vyenye kuijaza;+
12 Maeneo ya mashamba na vyote vyenye kuwa ndani yake vishangilie.+
Wakati uleule miti yote ya pori ipige vigelegele vya shangwe+
13 Mbele ya Yehova, kwa maana anakuja,*Anakuja kuhukumu dunia.
Atahukumu kwa haki dunia yenye kuikaliwa na watu*+Na vikundi vya watu kwa uaminifu wake.+

