Zaburi 112:1-10

  • Mwenye haki anamuogopa Yehova

    • Mutu mwenye kukopesha kwa ukarimu atasitawi (5)

    • “Mwenye haki atakumbukwa milele” (6)

    • Mutu mukarimu anapatiaka maskini (9)

112  Mumusifu Yah!*+ א [Aleph] Mwenye furaha ni mutu mwenye anamuogopa Yehova,+ב [Beth]Mwenye anapendezwa sana na amri zake.+ ג [Gimel]  2  Wazao wake watakuwa wenye nguvu katika dunia,ד [Daleth]Na kizazi cha watu wanyoofu kitabarikiwa.+ ה [He]  3  Mali na utajiri viko katika nyumba yake,ו [Waw]Na haki yake inadumu milele. ז [Zayin]  4  Anaangazia watu wanyoofu kama mwangaza katika giza.+ ח [Heth] Ni mwenye huruma,* mwenye rehema+ na mwenye haki. ט [Teth]  5  Mambo yanamuendea muzuri mutu mwenye kukopesha kwa ukarimu.*+ י [Yod] Anafanya mambo yake kwa haki. כ [Kaph]  6  Hatatikiswa hata kidogo.+ ל [Lamed] Mwenye haki atakumbukwa milele.+ מ [Mem]  7  Hataogopa habari ya mubaya.+ נ [Nun] Moyo wake uko imara, unamutegemea Yehova.+ ס [Samekh]  8  Moyo wake hauwezi kutikiswa;* haogope;+ע [Ayin]Mwishowe ataangalia kwa furaha kushindwa kwa maadui wake.+ פ [Pe]  9  Amegawa kwa wingi;* amepatia maskini.+ צ [Tsade] Haki yake inadumu milele.+ ק [Qoph] Nguvu zake mwenyewe zitainuliwa* kwa utukufu. ר [Resh] 10  Muovu ataona na kukasirika. ש [Shin] Atasaga meno yake na kuyeyuka. ת [Taw] Tamaa za waovu zitaangamia.+

Maelezo ya Chini

Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Ao “neema.”
Ao “neema.”
Ao “umeazimia; uko imara.”
Ao “kwa ukarimu.”
Tnn., “Pembe yake mwenyewe itainuliwa.”