Zaburi 12:1-8

  • Yehova anasimama ili kutenda

    • Maneno ya Mungu yako safi (6)

Kwa kiongozi; imepatanishwa na sauti ya Sheminiti.* Muziki wa Daudi. 12  Uniokoe, Ee Yehova, kwa maana mutu mushikamanifu haiko tena;Watu waaminifu hawako tena kati ya wana wa binadamu.  2  Wanaambiana uongo;Wanasifu-sifu kwa midomo yao* na kuzungumuza kwa mioyo midanganyifu.*+  3  Yehova atakata midomo yote yenye kusifu-sifuNa ulimi wenye kujisifu sana,+  4  Wale wenye kusema: “Tutashinda kupitia ndimi zetu. Tunatumia midomo yetu namna tunapenda;Ni nani atakuwa bwana wetu?”+  5  “Kwa sababu wale wenye kuteswa wanakandamizwa,Kwa sababu ya kilio cha maumivu cha maskini,+Nitasimama ili kutenda,” ni vile Yehova anasema. “Nitawaokoa kutoka kwa wale wenye kuwatendea kwa zarau.”*  6  Maneno ya Yehova yako safi;+Yako kama feza yenye ilisafishwa katika tanuru ya udongo,* yenye ilisafishwa mara saba (7).  7  Utawalinda, Ee Yehova;+Utamulinda kila mumoja wao milele kutokana na kizazi hiki.  8  Waovu wanatembea huku na huku bila kujizuiaKwa sababu wana wa binadamu wanaendeleza upotovu.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “Wanaongea kwa mudomo laini.”
Tnn., “kwa moyo na moyo.”
Ao “wenye wanajitutumua mbele yao.”
Ao pengine, “tanuru ya kuyeyusha yenye kuwekwa katika udongo.”