Zaburi 12:1-8
-
Yehova anasimama ili kutenda
-
Maneno ya Mungu yako safi (6)
-
Kwa kiongozi; imepatanishwa na sauti ya Sheminiti.* Muziki wa Daudi.
12 Uniokoe, Ee Yehova, kwa maana mutu mushikamanifu haiko tena;Watu waaminifu hawako tena kati ya wana wa binadamu.
2 Wanaambiana uongo;Wanasifu-sifu kwa midomo yao* na kuzungumuza kwa mioyo midanganyifu.*+
3 Yehova atakata midomo yote yenye kusifu-sifuNa ulimi wenye kujisifu sana,+
4 Wale wenye kusema: “Tutashinda kupitia ndimi zetu.
Tunatumia midomo yetu namna tunapenda;Ni nani atakuwa bwana wetu?”+
5 “Kwa sababu wale wenye kuteswa wanakandamizwa,Kwa sababu ya kilio cha maumivu cha maskini,+Nitasimama ili kutenda,” ni vile Yehova anasema.
“Nitawaokoa kutoka kwa wale wenye kuwatendea kwa zarau.”*
6 Maneno ya Yehova yako safi;+Yako kama feza yenye ilisafishwa katika tanuru ya udongo,* yenye ilisafishwa mara saba (7).
7 Utawalinda, Ee Yehova;+Utamulinda kila mumoja wao milele kutokana na kizazi hiki.
8 Waovu wanatembea huku na huku bila kujizuiaKwa sababu wana wa binadamu wanaendeleza upotovu.+

