Zaburi 11:1-7
Kwa kiongozi. Ya Daudi.
11 Nimemukimbilia Yehova.+
Basi namna gani munaweza kuniambia:*
“Kimbilia kwenye mulima wako kama ndege!
2 Angalia namna waovu wanakunja upinde;Wanatia mushale wao kwenye kamba ya upinde,Ili wapige kutoka katika giza wale wenye kuwa wanyoofu katika moyo.
3 Wakati misingi* inabomolewa,Mwenye haki anaweza kufanya nini?”
4 Yehova iko* katika hekalu lake takatifu.+
Kiti cha ufalme cha Yehova kiko mbinguni.+
Macho yake mwenyewe yanaangalia, macho yake yenye kuwa na uangalifu* yanachunguza wana wa binadamu.+
5 Yehova anachunguza mwenye haki na pia muovu;+Anachukia* mutu yeyote mwenye kupenda jeuri.+
6 Atanyeshea waovu mitego;*Moto na kiberiti+ na upepo wenye kuunguza vitakuwa fungu la kikombe chao.
7 Kwa maana Yehova ni mwenye haki;+ anapenda matendo yenye haki.+
Watu wanyoofu wataona uso wake.*+

