Zaburi 11:1-7

  • Kumukimbilia Yehova

    • “Yehova iko katika hekalu lake takatifu” (4)

    • Mungu anachukia mutu yeyote mwenye kupenda jeuri (5)

Kwa kiongozi. Ya Daudi. 11  Nimemukimbilia Yehova.+ Basi namna gani munaweza kuniambia:* “Kimbilia kwenye mulima wako kama ndege!  2  Angalia namna waovu wanakunja upinde;Wanatia mushale wao kwenye kamba ya upinde,Ili wapige kutoka katika giza wale wenye kuwa wanyoofu katika moyo.  3  Wakati misingi* inabomolewa,Mwenye haki anaweza kufanya nini?”  4  Yehova iko* katika hekalu lake takatifu.+ Kiti cha ufalme cha Yehova kiko mbinguni.+ Macho yake mwenyewe yanaangalia, macho yake yenye kuwa na uangalifu* yanachunguza wana wa binadamu.+  5  Yehova anachunguza mwenye haki na pia muovu;+Anachukia* mutu yeyote mwenye kupenda jeuri.+  6  Atanyeshea waovu mitego;*Moto na kiberiti+ na upepo wenye kuunguza vitakuwa fungu la kikombe chao.  7  Kwa maana Yehova ni mwenye haki;+ anapenda matendo yenye haki.+ Watu wanyoofu wataona uso wake.*+

Maelezo ya Chini

Ao “kuambia nafsi yangu.”
Ao “misingi ya haki.”
Ao “yenye kungaa.”
Ao “eko.”
Ao “Nafsi yake inachukia; Yeye mwenyewe anachukia.”
Ao pengine, “makaa yenye kuwaka.”
Ao “watajionea wema wake.”