Zaburi 25:1-22
Ya Daudi.
א [Aleph]
25 Ninageukia kwako,* Ee Yehova.
ב [Beth]
2 Mungu wangu, ninakutegemea wewe;+Usiruhusu nipatishwe haya.+
Usiruhusu maadui wangu washangilie juu ya magumu yangu.+
ג [Gimel]
3 Hakika hakuna mutu yeyote mwenye kukutumainia mwenye atapatishwa haya,+Lakini haya inangojea wale wenye kutenda kwa udanganyifu bila sababu.+
ד [Daleth]
4 Unijulishe njia zako, Ee Yehova;+Unifundishe mapito yako.+
ה [He]
5 Unitembeze katika kweli yako na unifundishe,+Kwa maana wewe ni Mungu wangu wa wokovu.
ו [Waw]
Ninakutumainia muchana wote.
ז [Zayin]
6 Kumbuka rehema yako, Ee Yehova, na upendo wako mushikamanifu,+Vyenye umeonyesha sikuzote.*+
ח [Heth]
7 Usikumbuke zambi zenye nilifanya wakati nilikuwa kijana na makosa yangu.
Unikumbuke kulingana na upendo wako mushikamanifu,+Kwa ajili ya wema wako, Ee Yehova.+
ט [Teth]
8 Yehova ni mwema na munyoofu.+
Ndiyo sababu anafundisha watenda-zambi namna ya kuishi.+
י [Yod]
9 Ataongoza wapole katika mambo yenye kuwa sawa,*+Na atafundisha wapole njia yake.+
כ [Kaph]
10 Njia za Yehova ni upendo mushikamanifu na uaminifuKwa ajili ya wale wenye kushika agano lake+ na vikumbusho vyake.+
ל [Lamed]
11 Kwa ajili ya jina lako, Ee Yehova,+Unisamehe kosa langu, hata kama ni kubwa.
מ [Mem]
12 Ni nani mwenye kumuogopa Yehova?+
Atamufundisha kuhusu njia yenye anapaswa kuchagua.+
נ [Nun]
13 Atajionea* mambo ya muzuri,+Na wazao wake watariti* dunia.+
ס [Samekh]
14 Urafiki wa karibu pamoja na Yehova ni wa wale wenye kumuogopa,+Na anawajulisha agano lake.+
ע [Ayin]
15 Macho yangu yanamuelekea Yehova sikuzote,+Kwa maana atatosha miguu yangu katika wavu.*+
פ [Pe]
16 Unielekezee uso wako na unionyeshe wema,Kwa maana niko peke yangu na sina uwezo.
צ [Tsade]
17 Taabu za moyo wangu zimeongezeka;+Unitoshe katika uchungu wangu.
ר [Resh]
18 Ona mateso yangu na taabu yangu,+Na usamehe zambi zangu zote.+
19 Angalia namna maadui wangu ni wengiNa namna wananichukia sana.
ש [Shin]
20 Linda uzima wangu* na uniokoe.+
Usiruhusu nipatishwe haya, kwa maana nimekukimbilia wewe.
ת [Taw]
21 Uaminifu-mushikamanifu na unyoofu vinilinde,+Kwa maana ninakutumainia wewe.+
22 Ee Mungu, okoa* Israeli katika taabu zake zote.

