Zaburi 146:1-10
146 Mumusifu Yah!*+
Nafsi yangu yote imusifu Yehova.+
2 Nitamusifu Yehova maisha yangu yote.
Nitamuimbia Mungu wangu sifa* wakati wote wenye nitakuwa muzima.
3 Musitumainie wakubwa*Wala mwana wa binadamu, mwenye hawezi kuleta wokovu.+
4 Roho* yake inatoka, anarudia kwenye udongo;+Siku ileile mawazo yake yanapotea.+
5 Mwenye furaha ni ule mwenye Mungu wa Yakobo ni musaidizi wake,+Mwenye anamutumainia Yehova Mungu wake,+
6 Mutengenezaji wa mbingu na dunia,Wa bahari, na vyote vyenye kuwa ndani,+Yeye mwenye kuwa muaminifu sikuzote,+
7 Yeye mwenye kutenda haki kwa ajili ya wale wenye walipunjwa,Yeye mwenye kupatia wenye njaa mukate.+
Yehova anaachilia huru wafungwa.+
8 Yehova anafungua macho ya vipofu;+Yehova anasimamisha wale wenye kuinama chini;+Yehova anapenda wenye haki.
9 Yehova analinda wakaaji wageni;Anamutegemeza mutoto mwenye hana baba na mujane,+Lakini anavunja mipango ya waovu.*+
10 Yehova atakuwa Mufalme milele,+Mungu wako, Ee Sayuni, kizazi kwa kizazi.
Mumusifu Yah!*

