Zaburi 85:1-13
Kwa kiongozi. Ya wana wa Kora.+ Muziki.
85 Ee Yehova, umeonyesha inchi yako wema;+Ulirudisha watu wa Yakobo wenye walikamatwa mateka.+
2 Umesamehe kosa la watu wako;Ulisamehe* zambi yao yote.+ (Sela)
3 Ulizuia gazabu yako yote;Uliacha kasirani yako kali.+
4 Uturudishe,* Ee Mungu wa wokovu wetu,Na uache kutukasirikia.+
5 Je, utatukasirikia sana milele?+
Je, utaendelea kukasirika kizazi kwa kizazi?
6 Je, hautatupatia tena uzimaIli watu wako washangilie katika wewe?+
7 Utuonyeshe upendo wako mushikamanifu, Ee Yehova,+Na utupatie wokovu wako.
8 Nitasikiliza jambo lenye Mungu wa kweli Yehova anasema,Kwa maana ataambia watu wake,+ washikamanifu wake, kuhusu amani,Lakini wasianze tena kujiaminia kupita kiasi.+
9 Hakika wokovu wake uko karibu na wale wenye kumuogopa,+Ili utukufu wake ukae katika inchi yetu.
10 Upendo mushikamanifu utakutana na uaminifu;Haki pamoja na amani vitapatiana busu.+
11 Uaminifu utachipuka katika dunia,Na haki itaangalia chini ikiwa mbinguni.+
12 Ndiyo, Yehova atatoa mambo ya muzuri,*+Na inchi yetu itazaa mavuno yake.+
13 Haki itatembea mbele yake+Na kutengeneza njia kwa ajili ya hatua zake.

