Zaburi 85:1-13

  • Sala ya kuomba warudishwe

    • Mungu ataambia washikamanifu wake kuhusu amani (8)

    • Upendo mushikamanifu utakutana na uaminifu (10)

Kwa kiongozi. Ya wana wa Kora.+ Muziki. 85  Ee Yehova, umeonyesha inchi yako wema;+Ulirudisha watu wa Yakobo wenye walikamatwa mateka.+  2  Umesamehe kosa la watu wako;Ulisamehe* zambi yao yote.+ (Sela)  3  Ulizuia gazabu yako yote;Uliacha kasirani yako kali.+  4  Uturudishe,* Ee Mungu wa wokovu wetu,Na uache kutukasirikia.+  5  Je, utatukasirikia sana milele?+ Je, utaendelea kukasirika kizazi kwa kizazi?  6  Je, hautatupatia tena uzimaIli watu wako washangilie katika wewe?+  7  Utuonyeshe upendo wako mushikamanifu, Ee Yehova,+Na utupatie wokovu wako.  8  Nitasikiliza jambo lenye Mungu wa kweli Yehova anasema,Kwa maana ataambia watu wake,+ washikamanifu wake, kuhusu amani,Lakini wasianze tena kujiaminia kupita kiasi.+  9  Hakika wokovu wake uko karibu na wale wenye kumuogopa,+Ili utukufu wake ukae katika inchi yetu. 10  Upendo mushikamanifu utakutana na uaminifu;Haki pamoja na amani vitapatiana busu.+ 11  Uaminifu utachipuka katika dunia,Na haki itaangalia chini ikiwa mbinguni.+ 12  Ndiyo, Yehova atatoa mambo ya muzuri,*+Na inchi yetu itazaa mavuno yake.+ 13  Haki itatembea mbele yake+Na kutengeneza njia kwa ajili ya hatua zake.

Maelezo ya Chini

Tnn., “Ulifunika.”
Ao “Utukusanye tena.”
Ao “mafanikio.”