Zaburi 80:1-19
Kwa kiongozi; imepatanishwa na “Maua ya Mayungiyungi.” Kikumbusho. Ya Asafu.+ Muziki.
80 Ee Muchungaji wa Israeli, sikiliza,Wewe mwenye kumuongoza Yosefu kama vile kundi.+
Wewe mwenye kukaa ukiwa mufalme juu ya* makerubi,+Angaza.*
2 Mbele ya Efraimu na Benyamini na Manase,Chochea nguvu zako;+Kuja na utuokoe.+
3 Ee Mungu, uturudishe;+Uso wako utuangazie, ili tuokolewe.+
4 Yehova Mungu wa majeshi, utaendelea mupaka wakati gani kuchukia* sala ya watu wako?+
5 Unawalisha machozi kama mukate,Na unawanywesha machozi kupita kipimo.
6 Unaruhusu majirani wetu wagombane kwa sababu yetu;Maadui wetu wanaendelea kutuchekelea namna wanapenda.+
7 Ee Mungu wa majeshi, uturudishe;Uso wako utuangazie, ili tuokolewe.+
8 Ulifanya muzabibu+ uondoke Misri.
Ulifukuza mataifa na kupanda muzabibu huo.+
9 Ulitayarisha nafasi kwa ajili yake,Nao ukatia mizizi na kujaa katika inchi.+
10 Milima ilifunikwa kwa kivuli chake,Na mierezi ya Mungu kwa matawi yake.
11 Matawi yake yalifika mupaka kwenye bahari,Na machipukizi yake mupaka kwenye ule Muto.*+
12 Sababu gani umebomoa kuta za majiwe za shamba la muzabibu huo,+Na hivyo wale wote wenye wanapita karibu nao wanachuma matunda yake?+
13 Nguruwe wa pori wanauharibu,Na wanyama wa pori wanaukula.+
14 Ee Mungu wa majeshi, rudia tafazali.
Angalia chini ukiwa mbinguni na uone!
Tunza muzabibu huu,+
15 Shina* lenye mukono wako wa kuume umepanda,+Na uangalie mwana mwenye* umemutia nguvu kwa ajili yako mwenyewe.+
16 Umeteketezwa kwa moto,+ umekatwa.
Wanaangamia kwa kemeo lako.*
17 Mukono wako umutegemeze mwanaume mwenye kuwa kwenye mukono wako wa kuume,Mwana wa binadamu mwenye umemutia nguvu kwa ajili yako mwenyewe.+
18 Kisha hatutageuka na kukuacha.
Linda uzima wetu, ili tuitie jina lako.
19 Ee Yehova Mungu wa majeshi, uturudishe;Uso wako utuangazie, ili tuokolewe.+

