Zaburi 87:1-7

  • Sayuni, muji wa Mungu wa kweli

    • Wenye walizaliwa Sayuni (4-6)

Ya wana wa Kora.+ Muziki. Wimbo. 87  Musingi wa muji wake uko katika milima mitakatifu.+  2  Yehova anapenda milango mikubwa ya Sayuni+Kuliko mahema yote ya Yakobo.  3  Mambo yenye utukufu yanasemwa kukuhusu, Ee muji wa Mungu wa kweli.+ (Sela)  4  Nitamuhesabia Rahabu+ na Babiloni kuwa kati ya wale wenye kunijua;*Angalia, Ufilisti na Tiro, pamoja na Kushi. Itasemwa: “Huyu alizaliwa kule.”  5  Na kuhusu Sayuni itasemwa: “Kila mumoja wao alizaliwa kule.” Na Mwenye Kuwa Juu Zaidi atamufanya kuwa imara kabisa.  6  Yehova atatangaza, wakati ataandikisha vikundi vya watu: “Huyu alizaliwa kule.” (Sela)  7  Waimbaji+ na wale wenye kucheza dansi za muzunguko+ watasema: “Chemchemi zangu zote ziko ndani yako.”*+

Maelezo ya Chini

Ao “kunitambua.”
Ao “Kwangu mimi, wewe uko chanzo cha vitu vyote.”