Zaburi 87:1-7
-
Sayuni, muji wa Mungu wa kweli
-
Wenye walizaliwa Sayuni (4-6)
-
Ya wana wa Kora.+ Muziki. Wimbo.
87 Musingi wa muji wake uko katika milima mitakatifu.+
2 Yehova anapenda milango mikubwa ya Sayuni+Kuliko mahema yote ya Yakobo.
3 Mambo yenye utukufu yanasemwa kukuhusu, Ee muji wa Mungu wa kweli.+ (Sela)
4 Nitamuhesabia Rahabu+ na Babiloni kuwa kati ya wale wenye kunijua;*Angalia, Ufilisti na Tiro, pamoja na Kushi.
Itasemwa: “Huyu alizaliwa kule.”
5 Na kuhusu Sayuni itasemwa:
“Kila mumoja wao alizaliwa kule.”
Na Mwenye Kuwa Juu Zaidi atamufanya kuwa imara kabisa.
6 Yehova atatangaza, wakati ataandikisha vikundi vya watu:
“Huyu alizaliwa kule.” (Sela)
7 Waimbaji+ na wale wenye kucheza dansi za muzunguko+ watasema:
“Chemchemi zangu zote ziko ndani yako.”*+