Zaburi 8:1-9

  • Utukufu wa Mungu na heshima ya mwanadamu

    • “Jina lako ni lenye utukufu sana!” (1,9)

    • ‘Mwanadamu mwenye anaweza kufa ni nini?’ (4)

    • Mwanadamu anavalishwa taji la utukufu (5)

Kwa kiongozi; juu ya Gititi.* Muziki wa Daudi. 8  Ee Yehova Bwana wetu, jina lako ni lenye utukufu sana katika dunia yote;Umetia utukufu wako juu zaidi hata kuliko mbingu!*+  2  Kutoka katika kinywa cha watoto na watoto wenye kunyonya+ umeimarisha nguvuKwa sababu ya maadui wako,Ili kumunyamazisha adui na mulipiza-kisasi.  3  Wakati ninaona mbingu zako, kazi za vidole vyako,Mwezi na nyota zenye umetayarisha,+  4  Mwanadamu mwenye anaweza kufa ni nini ili umuweke katika akili,Na mwana wa binadamu ili umuhangaikie?+  5  Ulimufanya kuwa mudogo kidogo kuliko wale wenye kuwa kama Mungu,*Na ulimuvalisha taji la utukufu na uzuri.  6  Ulimupatia mamlaka juu ya kazi za mikono yako;+Umeweka kila kitu chini ya miguu yake:  7  Makundi yote na ngombe wote,Na pia wanyama wa pori,+  8  Ndege wa mbinguni na samaki wa bahari,Kitu chochote chenye kinapita katika njia za bahari.  9  Ee Yehova Bwana wetu, jina lako ni lenye utukufu sana katika dunia yote!

Maelezo ya Chini

Ao pengine, “Wewe mwenye utukufu wako unasimuliwa juu ya mbingu!”
Ao “kuliko malaika.”