Zaburi 8:1-9
Kwa kiongozi; juu ya Gititi.*Muziki wa Daudi.
8 Ee Yehova Bwana wetu, jina lako ni lenye utukufu sana katika dunia yote;
Umetia utukufu wako juu zaidi hata kuliko mbingu!*+
2 Kutoka katika kinywa cha watoto na watoto wenye kunyonya+ umeimarisha nguvu
Kwa sababu ya maadui wako,
Ili kumunyamazisha adui na mulipiza-kisasi.
3 Wakati ninaona mbingu zako, kazi za vidole vyako,
Mwezi na nyota zenye umetayarisha,+
4 Mwanadamu mwenye anaweza kufa ni nini ili umuweke katika akili,
Na mwana wa binadamu ili umuhangaikie?+
5 Ulimufanya kuwa mudogo kidogo kuliko wale wenye kuwa kama Mungu,*
Na ulimuvalisha taji la utukufu na uzuri.
6 Ulimupatia mamlaka juu ya kazi za mikono yako;+
Umeweka kila kitu chini ya miguu yake:
7 Makundi yote na ngombe wote,
Na pia wanyama wa pori,+
8 Ndege wa mbinguni na samaki wa bahari,
Kitu chochote chenye kinapita katika njia za bahari.
9 Ee Yehova Bwana wetu, jina lako ni lenye utukufu sana katika dunia yote!
Maelezo ya Chini
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao pengine, “Wewe mwenye utukufu wako unasimuliwa juu ya mbingu!”
^ Ao “kuliko malaika.”