Zaburi 8:1-9

  • Utukufu wa Mungu na heshima ya mwanadamu

    • “Jina lako ni lenye utukufu sana!” (1, 9)

    • ‘Mwanadamu mwenye anaweza kufa ni nini?’ (4)

    • Mwanadamu anavalishwa taji la utukufu (5)

Kwa kiongozi; juu ya Gititi.*Muziki wa Daudi. 8  Ee Yehova Bwana wetu, jina lako ni lenye utukufu sana katika dunia yote; Umetia utukufu wako juu zaidi hata kuliko mbingu!*+   Kutoka katika kinywa cha watoto na watoto wenye kunyonya+ umeimarisha nguvu Kwa sababu ya maadui wako, Ili kumunyamazisha adui na mulipiza-kisasi.   Wakati ninaona mbingu zako, kazi za vidole vyako, Mwezi na nyota zenye umetayarisha,+   Mwanadamu mwenye anaweza kufa ni nini ili umuweke katika akili, Na mwana wa binadamu ili umuhangaikie?+   Ulimufanya kuwa mudogo kidogo kuliko wale wenye kuwa kama Mungu,* Na ulimuvalisha taji la utukufu na uzuri.   Ulimupatia mamlaka juu ya kazi za mikono yako;+ Umeweka kila kitu chini ya miguu yake:   Makundi yote na ngombe wote, Na pia wanyama wa pori,+   Ndege wa mbinguni na samaki wa bahari, Kitu chochote chenye kinapita katika njia za bahari.   Ee Yehova Bwana wetu, jina lako ni lenye utukufu sana katika dunia yote!

Maelezo ya Chini

Ao pengine, “Wewe mwenye utukufu wako unasimuliwa juu ya mbingu!”
Ao “kuliko malaika.”