Zaburi 46:1-11

  • “Mungu ni kimbilio letu”

    • Kazi za Mungu zenye kushangaza (8)

    • Mungu anamaliza vita katika dunia yote (9)

Kwa kiongozi. Ya wanawa Kora.+ Kulingana na mutindo waAlamoti.* Wimbo. 46  Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu,+Musaada wenye kupatikana kwa urahisi nyakati za taabu.+  2  Ndiyo sababu hatutaogopa, hata kama dunia inabadilika,Hata kama milima inaanguka katika sehemu za chini kabisa za bahari,+  3  Hata kama maji yake yananguruma na kutosha pofu nyingi,+Hata kama milima inatikiswa kwa sababu ya musukosuko wake. (Sela)  4  Kuko muto wenye mito yake midogo inafanya muji wa Mungu ushangilie,+Tabenakulo takatifu na kubwa ya Mwenye Kuwa Juu Zaidi.  5  Mungu iko* katika muji huo;+ hauwezi kupinduliwa. Mungu atausaidia wakati kunapambazuka.*+  6  Mataifa yalikuwa katika musukosuko, falme zilipinduliwa;Alipandisha sauti yake, na dunia ikayeyuka.+  7  Yehova wa majeshi iko* pamoja na sisi;+Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu salama.* (Sela)  8  Mukuje na mujionee matendo ya Yehova,Namna amefanya mambo yenye kushangaza katika dunia.  9  Anamaliza vita katika dunia yote.+ Anavunja upinde na kuvunja mukuki vipande-vipande;Anateketeza kwa moto magari ya kukokotwa ya vita.* 10  “Muache na mujue kwamba mimi ni Mungu. Nitatukuzwa kati ya mataifa;+Nitatukuzwa katika dunia.”+ 11  Yehova wa majeshi iko* pamoja na sisi;+Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu salama.+ (Sela)

Maelezo ya Chini

Ni kusema, wakati mwangaza wa asubui utaanza kutokea.
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Ao “mahali petu salama pa juu.”
Ao pengine, “ngao.”
Ao “eko.”