Zaburi 46:1-11
Kwa kiongozi. Ya wanawa Kora.+ Kulingana na mutindo waAlamoti.* Wimbo.
46 Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu,+Musaada wenye kupatikana kwa urahisi nyakati za taabu.+
2 Ndiyo sababu hatutaogopa, hata kama dunia inabadilika,Hata kama milima inaanguka katika sehemu za chini kabisa za bahari,+
3 Hata kama maji yake yananguruma na kutosha pofu nyingi,+Hata kama milima inatikiswa kwa sababu ya musukosuko wake. (Sela)
4 Kuko muto wenye mito yake midogo inafanya muji wa Mungu ushangilie,+Tabenakulo takatifu na kubwa ya Mwenye Kuwa Juu Zaidi.
5 Mungu iko* katika muji huo;+ hauwezi kupinduliwa.
Mungu atausaidia wakati kunapambazuka.*+
6 Mataifa yalikuwa katika musukosuko, falme zilipinduliwa;Alipandisha sauti yake, na dunia ikayeyuka.+
7 Yehova wa majeshi iko* pamoja na sisi;+Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu salama.* (Sela)
8 Mukuje na mujionee matendo ya Yehova,Namna amefanya mambo yenye kushangaza katika dunia.
9 Anamaliza vita katika dunia yote.+
Anavunja upinde na kuvunja mukuki vipande-vipande;Anateketeza kwa moto magari ya kukokotwa ya vita.*
10 “Muache na mujue kwamba mimi ni Mungu.
Nitatukuzwa kati ya mataifa;+Nitatukuzwa katika dunia.”+
11 Yehova wa majeshi iko* pamoja na sisi;+Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu salama.+ (Sela)

