Zaburi 93:1-5
93 Yehova amekuwa Mufalme!+
Amevaa utukufu;Yehova amevaa nguvu;Anazivaa kama mukaba.*
Dunia* imewekwa imara kabisa;Haiwezi kuhamishwa.*
2 Kiti chako cha ufalme kilifanywa kuwa imara kabisa zamani sana;+Tangu milele wewe uko.+
3 Mito imekuwa na mawimbi makubwa, Ee Yehova,Mito imekuwa na mawimbi makubwa na imenguruma;Mito inaendelea kuwa na mawimbi makubwa na kutoa kishindo.
4 Iko* na nguvu kuliko sauti ya maji mengi,Iko* na nguvu kuliko mawimbi makubwa ya bahari,+Yehova ni mukubwa katika nafasi za juu.+
5 Vikumbusho vyako vinategemeka sana.+
Utakatifu unapamba* nyumba yako+ nyakati zote, Ee Yehova.

