Zaburi 93:1-5
93 Yehova amekuwa Mufalme!+
Amevaa utukufu;
Yehova amevaa nguvu;
Anazivaa kama mukaba.*
Dunia* imewekwa imara kabisa;
Haiwezi kuhamishwa.*
2 Kiti chako cha ufalme kilifanywa kuwa imara kabisa zamani sana;+
Tangu milele wewe uko.+
3 Mito imekuwa na mawimbi makubwa, Ee Yehova,
Mito imekuwa na mawimbi makubwa na imenguruma;
Mito inaendelea kuwa na mawimbi makubwa na kutoa kishindo.
4 Iko* na nguvu kuliko sauti ya maji mengi,
Iko* na nguvu kuliko mawimbi makubwa ya bahari,+
Yehova ni mukubwa katika nafasi za juu.+
5 Vikumbusho vyako vinategemeka sana.+
Utakatifu unapamba* nyumba yako+ nyakati zote, Ee Yehova.
Maelezo ya Chini
^ Ao “mushipi.”
^ Ao “Inchi yenye kuzaa.”
^ Ao “kutikisika.”
^ Ao “Eko.”
^ Ao “Eko.”
^ Ao “unafaa.”