Zaburi 19:1-14

  • Uumbaji wa Mungu na sheria yake vinatoa ushahidi

    • ‘Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu’ (1)

    • Sheria kamilifu ya Mungu inarudisha nguvu (7)

    • “Zambi zenye sijue” (12)

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi. 19  Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu;+Na anga lenye kuwa juu linatangaza kazi ya mikono yake.+  2  Siku kwa siku maneno yavyo yanabubujika,Na usiku kwa usiku vinafunua ujuzi.  3  Hakuna usemi, na hakuna maneno;Sauti yao haisikike.  4  Lakini sauti yao* imefika katika dunia yote,Na ujumbe wao mupaka kwenye miisho ya dunia yenye kuikaliwa na watu.*+ Amesimamisha hema mbinguni kwa ajili ya jua;  5  Ni kama bwana-arusi mwenye anatoka katika chumba chake cha arusi;Linashangilia kama mwanaume mwenye nguvu mwenye anakimbia kwenye njia yake.  6  Linatokea kwenye mwisho mumoja wa mbingu,Na linazunguka mupaka mwisho mwingine wa mbingu;+Na hakuna kitu chochote chenye kinafichwa kisipatwe na joto lake.  7  Sheria ya Yehova ni kamilifu,+ inarudisha nguvu.*+ Kikumbusho cha Yehova kinategemeka,+ kinamufanya mwenye hana uzoefu akuwe na hekima.+  8  Maagizo kutoka kwa Yehova ni yenye haki, yanafanya moyo ushangilie;+Amri ya Yehova ni safi, inafanya macho yangae.+  9  Kumuogopa Yehova+ ni jambo safi, kunadumu milele. Hukumu za Yehova ni za kweli; zote ni zenye haki.+ 10  Ni zenye kutamanika zaidi kuliko zahabu,Kuliko zahabu nyingi safi,*+Na ziko tamu zaidi kuliko asali,+ asali yenye kuanguka matone-matone kutoka katika sega. 11  Mutumishi wako ameonywa kupitia hizo;+Katika kuzishika, kuko zawabu kubwa.+ 12  Ni nani anaweza kutambua makosa?+ Unitangaze kuwa sina hatia ya zambi zenye sijue. 13  Na umuzuie mutumishi wako asitende matendo ya kimbelembele;+Usiruhusu yanitawale.+ Halafu nitakuwa kamili,+Na sitakuwa na hatia ya zambi zenye kuwa wazi.* 14  Maneno ya kinywa changu na kufikiri sana* kwa moyo wanguVikupendeze wewe,+ Ee Yehova, Mwamba wangu+ na Mukombozi wangu.+

Maelezo ya Chini

Ao pengine, “kamba yao ya kupimia.”
Ao “inchi yenye kuzaa.”
Ao “inarudisha nafsi.”
Ao “yenye ilisafishwa.”
Ao “makosa mengi.”
Ao “kutafakari.”