Zaburi 124:1-8

  • “Kama Yehova hangekuwa pamoja na sisi”

    • Ponyoka mutego wenye ulivunjika (7)

    • ‘Jina la Yehova ni musaada wetu’ (8)

Wimbo wa Safari za Kupanda. Wa Daudi. 124  “Kama Yehova hangekuwa pamoja na sisi”+​—⁠Israeli aseme sasa⁠—  2  “Kama Yehova hangekuwa pamoja na sisi+Wakati watu walisimama ili kutushambulia,+  3  Basi wangetumeza tukiwa wazima+Wakati kasirani yao ilikuwa inawaka juu yetu.+  4  Kisha maji yangetufagilia mbali,Maji mengi yangetufunika.*+  5  Maji yenye nguvu yangetulemea.*  6  Yehova asifiwe,Kwa maana hakututia katika meno yao kama mawindo.  7  Tuko* kama ndege mwenye aliponyokaKatika mutego wa muwindaji;+Mutego ulivunjika,Na sisi tukaponyoka.+  8  Musaada wetu uko katika jina la Yehova,+Mutengenezaji wa mbingu na dunia.”

Maelezo ya Chini

Ao “yangefunika nafsi yetu.”
Ao “yangelemea nafsi yetu.”
Ao “Nafsi yetu iko.”