Zaburi 124:1-8

  • “Kama Yehova hangekuwa pamoja na sisi”

    • Ponyoka mutego wenye ulivunjika (7)

    • ‘Jina la Yehova ni musaada wetu’ (8)

Wimbo wa Safari za Kupanda. Wa Daudi. 124  “Kama Yehova hangekuwa pamoja na sisi”+ —Israeli aseme sasa—   “Kama Yehova hangekuwa pamoja na sisi+ Wakati watu walisimama ili kutushambulia,+   Basi wangetumeza tukiwa wazima+ Wakati kasirani yao ilikuwa inawaka juu yetu.+   Kisha maji yangetufagilia mbali, Maji mengi yangetufunika.*+   Maji yenye nguvu yangetulemea.*   Yehova asifiwe, Kwa maana hakututia katika meno yao kama mawindo.   Tuko* kama ndege mwenye aliponyoka Katika mutego wa muwindaji;+ Mutego ulivunjika, Na sisi tukaponyoka.+   Musaada wetu uko katika jina la Yehova,+ Mutengenezaji wa mbingu na dunia.”

Maelezo ya Chini

Ao “yangefunika nafsi yetu.”
Ao “yangelemea nafsi yetu.”
Ao “Nafsi yetu iko.”