Zaburi 124:1-8
Wimbo wa Safari za Kupanda. Wa Daudi.
124 “Kama Yehova hangekuwa pamoja na sisi”+
—Israeli aseme sasa—
2 “Kama Yehova hangekuwa pamoja na sisi+
Wakati watu walisimama ili kutushambulia,+
3 Basi wangetumeza tukiwa wazima+
Wakati kasirani yao ilikuwa inawaka juu yetu.+
4 Kisha maji yangetufagilia mbali,
Maji mengi yangetufunika.*+
5 Maji yenye nguvu yangetulemea.*
6 Yehova asifiwe,
Kwa maana hakututia katika meno yao kama mawindo.
7 Tuko* kama ndege mwenye aliponyoka
Katika mutego wa muwindaji;+
Mutego ulivunjika,
Na sisi tukaponyoka.+
8 Musaada wetu uko katika jina la Yehova,+
Mutengenezaji wa mbingu na dunia.”
Maelezo ya Chini
^ Ao “yangefunika nafsi yetu.”
^ Ao “yangelemea nafsi yetu.”
^ Ao “Nafsi yetu iko.”