Zaburi 126:1-6

  • Sayuni itarudishwa kwa shangwe

    • ‘Yehova ametenda mambo makubwa’ (3)

    • Kisha kulia, kutakuwa shangwe (5, 6)

Wimbo wa Safari za Kupanda. 126  Wakati Yehova alikusanya na kurudisha watu wenye walikamatwa mateka wa Sayuni,+Tuliwaza tulikuwa tunaota ndoto.  2  Wakati huo kinywa chetu kilijaa kichekoNa ulimi wetu vigelegele vya shangwe.+ Wakati huo walisema kati ya mataifa: “Yehova amewatendea mambo makubwa.”+  3  Yehova ametutendea mambo makubwa,+Na tuko na furaha kubwa sana.  4  Kusanya na urudishe watu wetu wenye walikamatwa mateka, Ee Yehova,Kama mito midogo ya Negebu.*  5  Wale wenye kupanda mbegu kwa machoziWatavuna kwa vigelegele vya shangwe.  6  Ule mwenye anaenda inje, hata kama iko* analia,Akiwa amebeba mufuko wake wa mbegu,Hakika atarudia kwa vigelegele vya shangwe,+Akiwa amebeba mafungu yake ya mbegu.+

Maelezo ya Chini

Ao “mabonde ya kusini.”
Ao “eko.”