Zaburi 142:1-7

  • Sala ya kuomba aokolewe kutoka kwa watesaji

    • “Hakuna kwenye ninaweza kukimbilia” (4)

    • “Sina mwingine isipokuwa wewe” (5)

Maskili.* Ya Daudi, wakati alikuwa katika pango.+ Sala. 142  Kwa sauti yangu ninamuita Yehova anisaidie;+Kwa sauti yangu ninamulilia Yehova anionyeshe wema.  2  Mbele yake ninamwanga mahangaiko yangu;Mbele yake ninaeleza taabu yangu+  3  Wakati roho yangu inazimia ndani yangu.* Kisha unaangalia barabara yangu.+ Katika njia kwenye ninatembea,Wanaficha mutego wa kuninasa.  4  Angalia kwenye mukono wangu wa kuume na uoneKwamba hakuna mwenye ananihangaikia.*+ Hakuna kwenye ninaweza kukimbilia;+Hakuna mwenye ananihangaikia.*  5  Ninakuita unisaidie, Ee Yehova. Ninasema: “Wewe ni kimbilio langu,+Sina mwingine isipokuwa wewe* katika inchi ya wazima.”  6  Sikiliza kilio changu cha kuomba musaada,Kwa maana nimeshushwa chini sana. Uniokoe kutoka kwa wale wenye kunitesa,+Kwa maana ni wenye nguvu kuliko mimi.  7  Unitoshe* katika gereza la chini ya udongoIli nisifu jina lako. Wenye haki wakusanyike kunizungukaKwa sababu unanitendea kwa fazili.

Maelezo ya Chini

Ao “Wakati nguvu zinaniisha.”
Tnn., “ananitambua.”
Ao “anahangaikia nafsi yangu.”
Tnn., “Fungu langu.”
Ao “Tosha nafsi yangu.”