Zaburi 142:1-7
Maskili.* Ya Daudi, wakati alikuwa katika pango.+ Sala.
142 Kwa sauti yangu ninamuita Yehova anisaidie;+Kwa sauti yangu ninamulilia Yehova anionyeshe wema.
2 Mbele yake ninamwanga mahangaiko yangu;Mbele yake ninaeleza taabu yangu+
3 Wakati roho yangu inazimia ndani yangu.*
Kisha unaangalia barabara yangu.+
Katika njia kwenye ninatembea,Wanaficha mutego wa kuninasa.
4 Angalia kwenye mukono wangu wa kuume na uoneKwamba hakuna mwenye ananihangaikia.*+
Hakuna kwenye ninaweza kukimbilia;+Hakuna mwenye ananihangaikia.*
5 Ninakuita unisaidie, Ee Yehova.
Ninasema: “Wewe ni kimbilio langu,+Sina mwingine isipokuwa wewe* katika inchi ya wazima.”
6 Sikiliza kilio changu cha kuomba musaada,Kwa maana nimeshushwa chini sana.
Uniokoe kutoka kwa wale wenye kunitesa,+Kwa maana ni wenye nguvu kuliko mimi.
7 Unitoshe* katika gereza la chini ya udongoIli nisifu jina lako.
Wenye haki wakusanyike kunizungukaKwa sababu unanitendea kwa fazili.

