Zaburi 142:1-7
Maskili.* Ya Daudi, wakati alikuwa katika pango.+ Sala.
142 Kwa sauti yangu ninamuita Yehova anisaidie;+
Kwa sauti yangu ninamulilia Yehova anionyeshe wema.
2 Mbele yake ninamwanga mahangaiko yangu;
Mbele yake ninaeleza taabu yangu+
3 Wakati roho yangu inazimia ndani yangu.*
Kisha unaangalia barabara yangu.+
Katika njia kwenye ninatembea,
Wanaficha mutego wa kuninasa.
4 Angalia kwenye mukono wangu wa kuume na uone
Kwamba hakuna mwenye ananihangaikia.*+
Hakuna kwenye ninaweza kukimbilia;+
Hakuna mwenye ananihangaikia.*
5 Ninakuita unisaidie, Ee Yehova.
Ninasema: “Wewe ni kimbilio langu,+
Sina mwingine isipokuwa wewe* katika inchi ya wazima.”
6 Sikiliza kilio changu cha kuomba musaada,
Kwa maana nimeshushwa chini sana.
Uniokoe kutoka kwa wale wenye kunitesa,+
Kwa maana ni wenye nguvu kuliko mimi.
7 Unitoshe* katika gereza la chini ya udongo
Ili nisifu jina lako.
Wenye haki wakusanyike kunizunguka
Kwa sababu unanitendea kwa fazili.
Maelezo ya Chini
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “Wakati nguvu zinaniisha.”
^ Tnn., “ananitambua.”
^ Ao “anahangaikia nafsi yangu.”
^ Tnn., “Fungu langu.”
^ Ao “Tosha nafsi yangu.”