Zaburi 70:1-5

  • Anaomba asaidiwe haraka

    • “Tenda haraka kwa ajili yangu” (5)

Kwa kiongozi. Ya Daudi,ya kukumbusha. 70  Ee Mungu, uniokoe;Ee Yehova, fanya haraka ili unisaidie.+  2  Acha wale wenye kutafuta kuondoa uzima wangu*Wapatishwe haya na kufezeheshwa. Acha wale wenye kufurahia musiba wanguWakimbie kwa sababu ya aibu.  3  Acha wale wenye kusema: “Aha! Aha!” Wakimbizwe kwa sababu ya haya.  4  Lakini acha wale wenye kukutafutaWafurahi na kushangilia katika wewe.+ Acha wale wenye kupenda matendo yako ya wokovu waseme sikuzote: “Mungu atukuzwe!”  5  Lakini mimi sina uwezo na niko maskini;+Ee Mungu, tenda haraka kwa ajili yangu.+ Wewe ni musaidizi wangu na mwokozi wangu.+ Ee Yehova, usikawie.+

Maelezo ya Chini

Ao “nafsi yangu.”