Zaburi 70:1-5

  • Anaomba asaidiwe haraka

    • “Tenda haraka kwa ajili yangu” (5)

Kwa kiongozi. Ya Daudi,ya kukumbusha. 70  Ee Mungu, uniokoe; Ee Yehova, fanya haraka ili unisaidie.+   Acha wale wenye kutafuta kuondoa uzima wangu* Wapatishwe haya na kufezeheshwa. Acha wale wenye kufurahia musiba wangu Wakimbie kwa sababu ya aibu.   Acha wale wenye kusema: “Aha! Aha!” Wakimbizwe kwa sababu ya haya.   Lakini acha wale wenye kukutafuta Wafurahi na kushangilia katika wewe.+ Acha wale wenye kupenda matendo yako ya wokovu waseme sikuzote: “Mungu atukuzwe!”   Lakini mimi sina uwezo na niko maskini;+ Ee Mungu, tenda haraka kwa ajili yangu.+ Wewe ni musaidizi wangu na mwokozi wangu.+ Ee Yehova, usikawie.+

Maelezo ya Chini

Ao “nafsi yangu.”