Zaburi 70:1-5
-
Anaomba asaidiwe haraka
-
“Tenda haraka kwa ajili yangu” (5)
-
Kwa kiongozi. Ya Daudi,ya kukumbusha.
70 Ee Mungu, uniokoe;
Ee Yehova, fanya haraka ili unisaidie.+
2 Acha wale wenye kutafuta kuondoa uzima wangu*
Wapatishwe haya na kufezeheshwa.
Acha wale wenye kufurahia musiba wangu
Wakimbie kwa sababu ya aibu.
3 Acha wale wenye kusema: “Aha! Aha!”
Wakimbizwe kwa sababu ya haya.
4 Lakini acha wale wenye kukutafuta
Wafurahi na kushangilia katika wewe.+
Acha wale wenye kupenda matendo yako ya wokovu waseme sikuzote:
“Mungu atukuzwe!”
5 Lakini mimi sina uwezo na niko maskini;+
Ee Mungu, tenda haraka kwa ajili yangu.+
Wewe ni musaidizi wangu na mwokozi wangu.+
Ee Yehova, usikawie.+
Maelezo ya Chini
^ Ao “nafsi yangu.”