ULIZO LA 6
Biblia Ilitabiri Nini Juu ya Masiya?
UNABII
“Wewe, Ee Betlehemu Efrata, . . . mwenye atatawala katika Israeli kwa ajili yangu atatokea kwako.”
UTIMIZO
“Kisha Yesu kuzaliwa katika Betlehemu ya Yudea katika siku za mufalme Herode, angalia! watu wenye elimu ya nyota kutoka Mashariki walikuja Yerusalemu.”
UNABII
“Wanagawana nguo zangu kati yao wenyewe, na wanapigia nguo zangu kura.”
UTIMIZO
“Sasa, kisha maaskari kumupigilia Yesu misumari kwenye muti, wakakamata nguo zake za inje na kuzigawanya katika sehemu ine (4) . . . Lakini nguo hiyo ya ndani haikukuwa na mushono, ilikuwa imesukwa kuanzia juu mupaka chini. Basi wakaambiana: ‘Tusiipasue, lakini tuipigie kura ili kuamua itakuwa ya nani.’”
UNABII
“Analinda mifupa yake yote; hakuna mumoja kati ya mifupa yake wenye umevunjwa.”
UTIMIZO
“Wakati walikuja kwa Yesu, waliona kwamba alikuwa amekwisha kufa, kwa hiyo hawakuvunja miguu yake.”
UNABII
“Alitobolewa kwa silaha kwa ajili ya ukosaji wetu.”
UTIMIZO
“Mumoja wa maaskari akamuingiza mukuki kwenye ubavu, na mara moja damu na maji vikatoka.”
UNABII
“Wakalipa malipo yangu, vipande makumi tatu (30) vya feza.”
UTIMIZO
“Kisha mumoja wa wale Kumi na Mbili (12), ule mwenye aliitwa Yuda Iskariote, akaenda kwa wakubwa wa makuhani na kusema: ‘Mutanipatia nini ili nimusaliti kwenu?’ Wakasikilizana kumupatia vipande makumi tatu (30) vya feza.”