Zaburi 148:1-14
148 Mumusifu Yah!*
Mumusifu Yehova kutoka mbinguni,+Mumusifu katika nafasi za juu.
2 Mumusifu, ninyi malaika wake wote.+
Mumusifu, ninyi jeshi lake lote.+
3 Mumusifu, jua na mwezi.
Mumusifu, nyota zote zenye kungaa.+
4 Mumusifu, Enyi mbingu zenye kuwa juu sana*Na maji yenye kuwa juu ya mbingu.
5 Visifu jina la Yehova,Kwa maana aliamuru, na vikaumbwa.+
6 Anavifanya viendelee kuwa imara milele na milele;+Ametoa agizo lenye halitapita.+
7 Mumusifu Yehova kutoka katika dunia,Ninyi viumbe vikubwa vya bahari na maji yote yenye kuenda chini sana,
8 Ninyi umeme wa radi na mvua ya majiwe, teluji* na mawingu mazito,Wewe upepo wa zoruba, ninyi wenye kutenda neno lake,+
9 Ninyi milima na vilima vyote,+Ninyi miti ya matunda na mierezi yote,+
10 Ninyi wanyama wa pori+ na wanyama wote wa kufugwa,Ninyi viumbe vyenye kutambaa na ndege wenye mabawa,
11 Ninyi wafalme wa dunia, na ninyi mataifa yote,Ninyi wakubwa na waamuzi wote wa dunia,+
12 Ninyi vijana wanaume na vijana wanamuke,*Wazee pamoja na vijana.
13 Wasifu jina la Yehova,Kwa maana jina lake peke yake liko juu sana haliwezi kufikiwa.+
Ukubwa wake uko juu ya dunia na mbingu.+
14 Atainua nguvu* ya watu wake,Kwa ajili ya sifa ya washikamanifu wake wote,Ya wana wa Israeli, watu wenye kuwa karibu naye.
Mumusifu Yah!*

