Zaburi 148:1-14

  • Uumbaji wote umusifu Yehova

    • “Mumusifu, ninyi malaika wake wote” (2)

    • ‘Mumusifu, jua, mwezi, na nyota’ (3)

    • Vijana na wazee wamusifu Mungu (12, 13)

148  Mumusifu Yah!* Mumusifu Yehova kutoka mbinguni,+Mumusifu katika nafasi za juu.  2  Mumusifu, ninyi malaika wake wote.+ Mumusifu, ninyi jeshi lake lote.+  3  Mumusifu, jua na mwezi. Mumusifu, nyota zote zenye kungaa.+  4  Mumusifu, Enyi mbingu zenye kuwa juu sana*Na maji yenye kuwa juu ya mbingu.  5  Visifu jina la Yehova,Kwa maana aliamuru, na vikaumbwa.+  6  Anavifanya viendelee kuwa imara milele na milele;+Ametoa agizo lenye halitapita.+  7  Mumusifu Yehova kutoka katika dunia,Ninyi viumbe vikubwa vya bahari na maji yote yenye kuenda chini sana,  8  Ninyi umeme wa radi na mvua ya majiwe, teluji* na mawingu mazito,Wewe upepo wa zoruba, ninyi wenye kutenda neno lake,+  9  Ninyi milima na vilima vyote,+Ninyi miti ya matunda na mierezi yote,+ 10  Ninyi wanyama wa pori+ na wanyama wote wa kufugwa,Ninyi viumbe vyenye kutambaa na ndege wenye mabawa, 11  Ninyi wafalme wa dunia, na ninyi mataifa yote,Ninyi wakubwa na waamuzi wote wa dunia,+ 12  Ninyi vijana wanaume na vijana wanamuke,*Wazee pamoja na vijana. 13  Wasifu jina la Yehova,Kwa maana jina lake peke yake liko juu sana haliwezi kufikiwa.+ Ukubwa wake uko juu ya dunia na mbingu.+ 14  Atainua nguvu* ya watu wake,Kwa ajili ya sifa ya washikamanifu wake wote,Ya wana wa Israeli, watu wenye kuwa karibu naye. Mumusifu Yah!*

Maelezo ya Chini

Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Tnn., “mbingu za mbingu.”
Ao “neige.”
Tnn., “mabikira.”
Tnn., “pembe.”
Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.