Zaburi 55:1-23
Kwa kiongozi; iimbwe kwa vyombo vya kamba. Maskili.* Ya Daudi.
55 Sikiliza sala yangu, Ee Mungu,+Na usipuuze sala yangu ya kuomba rehema.*+
2 Unisikilize na unijibu.+
Hangaiko langu linanifanya nikose utulivu,+Na nimevurugika
3 Kwa sababu ya mambo yenye adui anasemaNa mukazo kutoka kwa muovu.
Kwa maana wanarundika taabu juu yangu,Na kwa kasirani wananiwekea chuki.+
4 Moyo wangu uko katika uchungu ndani yangu,+Na hofu za kifo zinanilemea.+
5 Woga na kutetemeka vinakuja juu yangu,Na kutetemeka kunanishika.
6 Ninaendelea kusema: “Kama tu ningekuwa na mabawa kama njiwa!
Ningeruka mbali na kukaa kwa usalama.
7 Angalia! Ningekimbia na kuenda mbali sana.+
Ningekaa katika jangwa.+ (Sela)
8 Ningeenda haraka mahali pa kujifichaMbali na upepo mukali, mbali na zoruba.”
9 Uwavuruge, Ee Yehova, na uvuruge mipango yao,*+Kwa maana nimeona jeuri na muzozo katika muji.
10 Usiku na muchana wanazunguka juu ya kuta zake;Ndani yake kuko nia mubaya na taabu.+
11 Uharibifu uko ndani yake;Ukandamizaji na udanganyifu haviondoke hata kidogo katika kiwanja chake cha watu wote.+
12 Kwa maana haiko adui ndiye ananichokoza;+Ingekuwa vile ningevumilia.
Haiko adui ndiye amesimama ili kunishambulia;Ingekuwa vile ningejificha asinipate.
13 Lakini ni wewe, mwanadamu kama mimi,*+Rafiki yangu mwenyewe ambaye ninajua muzuri.+
14 Tulikuwa tunafurahia pamoja urafiki wa karibu sana;Katika nyumba ya Mungu tulikuwa tunatembea pamoja na kikundi cha watu.
15 Uharibifu uwapate!+
Washuke katika Kaburi* wakiwa wazima;Kwa maana uovu unakaa kati yao na ndani yao.
16 Lakini mimi, nitamuita Mungu,Na Yehova ataniokoa.+
17 Mangaribi na asubui na katikati ya muchana, ninahangaika na kulia kwa maumivu,*+Na anasikia sauti yangu.+
18 Ataniokoa* na kunipatia* amani mbali na wale wenye kupigana na mimi,Kwa maana vikundi vya watu vinakuja kunishambulia.+
19 Mungu atasikia na kuwajibu,+Ule mwenye kukaa akiwa mufalme tangu zamani.+ (Sela)
Watakataa kubadilika,Wale wenye hawajamuogopa Mungu.+
20 Yeye* alishambulia wale wenye kuishi kwa amani pamoja naye;+Alivunja agano lake.+
21 Maneno yake ni laini kuliko siagi,+Lakini muzozo uko katika moyo wake.
Maneno yake ni laini kuliko mafuta,Lakini ni panga zenye kuchomolewa.+
22 Umutupie Yehova muzigo wako,+Naye atakutegemeza.+
Hataruhusu hata kidogo mwenye haki aanguke.*+
23 Lakini wewe, Ee Mungu, utawashusha chini kwenye shimo la murefu kabisa.+
Watu hao wenye hatia ya damu wenye ni wadanganyifu hawataishi nusu ya siku zao.+
Lakini mimi, nitakutegemea wewe.
Maelezo ya Chini
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “Na usijifiche wakati ninasali ili kukuomba musaada.”
^ Tnn., “ugawanye ulimi wao.”
^ Ao “mwanadamu, mutu mwenye kuwa sawa na mimi.”
^ Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “nimevurugika.”
^ Tnn., “Atanikomboa.”
^ Ao “kupatia nafsi yangu.”
^ Ni kusema, ule rafiki wa zamani mwenye kutajwa katika mustari wa 13 na 14.
^ Ao “ayumbe-yumbe.”