Zaburi 30:1-12
-
Maombolezo yanageuzwa kuwa shangwe
-
Wema wa Mungu unadumu maisha yote (5)
-
Muziki. Wimbo wa kuzindua nyumba. Wa Daudi.
30 Nitakutukuza, Ee Yehova, kwa maana umeniinua* juu;
Haukuruhusu maadui wangu washangilie juu yangu.+
2 Ee Yehova Mungu wangu, nilikulilia unisaidie, na wewe ukaniponyesha.+
3 Ee Yehova, umeniinua* kutoka katika Kaburi.*+
Ulilinda uzima wangu; uliniokoa nisizame katika shimo.*+
4 Mumuimbie Yehova sifa,* ninyi washikamanifu wake,+
Mushukuru jina lake takatifu;*+
5 Kwa sababu kuwa chini ya kasirani yake ni kwa wakati mufupi tu,+
Lakini kuwa katika wema wake* kunadumu maisha yote.+
Kilio kinaweza kutokea mangaribi, lakini asubui, vigelegele vya shangwe.+
6 Wakati nilikuwa na amani, nilisema:
“Sitatikiswa* hata kidogo.”
7 Ee Yehova, wakati nilikuwa katika wema wako,* ulinifanya imara kama mulima.+
Lakini wakati ulificha uso wako, niliogopa sana.+
8 Niliendelea kukuita, Ee Yehova;+
Na niliendelea kumulilia Yehova ili anionyeshe wema.
9 Kuko faida gani kama ninakufa,* kama ninashuka katika shimo?*+
Je, mavumbi yatakusifu?+ Je, yataongea kuhusu uaminifu wako?+
10 Sikia, Ee Yehova, na unionyeshe wema.+
Ee Yehova, ukuwe musaidizi wangu.+
11 Umegeuza maombolezo yangu kuwa dansi;
Umenitosha nguo yangu ya gunia, na unanivalisha shangwe,
12 Ili niimbe* sifa yako na nisinyamaze.
Ee Yehova Mungu wangu, nitakusifu milele.
Maelezo ya Chini
^ Ao “umenivuta.”
^ Ao “umeinua nafsi yangu.”
^ Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “kaburi.”
^ Ao “Mumupigie Yehova muziki.”
^ Tnn., “ukumbusho wake.”
^ Ao “kuwa chini ya nia yake njema.”
^ Ao “Sitayumba-yumba.”
^ Ao “nilikuwa katika nia yako njema.”
^ Tnn., “Damu yangu iko na faida gani.”
^ Ao “kaburi.”
^ Ao “Ili utukufu wangu uimbe.”