Zaburi 30:1-12

  • Maombolezo yanageuzwa kuwa shangwe

    • Wema wa Mungu unadumu maisha yote (5)

Muziki. Wimbo wa kuzindua nyumba. Wa Daudi. 30  Nitakutukuza, Ee Yehova, kwa maana umeniinua* juu; Haukuruhusu maadui wangu washangilie juu yangu.+   Ee Yehova Mungu wangu, nilikulilia unisaidie, na wewe ukaniponyesha.+   Ee Yehova, umeniinua* kutoka katika Kaburi.*+ Ulilinda uzima wangu; uliniokoa nisizame katika shimo.*+   Mumuimbie Yehova sifa,* ninyi washikamanifu wake,+ Mushukuru jina lake takatifu;*+   Kwa sababu kuwa chini ya kasirani yake ni kwa wakati mufupi tu,+ Lakini kuwa katika wema wake* kunadumu maisha yote.+ Kilio kinaweza kutokea mangaribi, lakini asubui, vigelegele vya shangwe.+   Wakati nilikuwa na amani, nilisema: “Sitatikiswa* hata kidogo.”   Ee Yehova, wakati nilikuwa katika wema wako,* ulinifanya imara kama mulima.+ Lakini wakati ulificha uso wako, niliogopa sana.+   Niliendelea kukuita, Ee Yehova;+ Na niliendelea kumulilia Yehova ili anionyeshe wema.   Kuko faida gani kama ninakufa,* kama ninashuka katika shimo?*+ Je, mavumbi yatakusifu?+ Je, yataongea kuhusu uaminifu wako?+ 10  Sikia, Ee Yehova, na unionyeshe wema.+ Ee Yehova, ukuwe musaidizi wangu.+ 11  Umegeuza maombolezo yangu kuwa dansi; Umenitosha nguo yangu ya gunia, na unanivalisha shangwe, 12  Ili niimbe* sifa yako na nisinyamaze. Ee Yehova Mungu wangu, nitakusifu milele.

Maelezo ya Chini

Ao “umenivuta.”
Ao “umeinua nafsi yangu.”
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Ao “kaburi.”
Ao “Mumupigie Yehova muziki.”
Tnn., “ukumbusho wake.”
Ao “kuwa chini ya nia yake njema.”
Ao “Sitayumba-yumba.”
Ao “nilikuwa katika nia yako njema.”
Tnn., “Damu yangu iko na faida gani.”
Ao “kaburi.”
Ao “Ili utukufu wangu uimbe.”