Zaburi 9:1-20
Kwa kiongozi; juu ya Mut-labeni.* Muziki wa Daudi.
א [Aleph]
9 Nitakusifu, Ee Yehova, kwa moyo wangu wote;Nitazungumuza kuhusu kazi zako zote za ajabu.+
2 Nitafurahi na kushangilia katika wewe;Nitaimbia jina lako sifa,* Ee Mwenye Kuwa Juu Zaidi.+
ב [Beth]
3 Wakati maadui wangu wanakimbia,+Watajikwaa na kuangamia wasikuwe tena mbele yako.
4 Kwa maana unatetea njia yangu ya haki;Unakaa kwenye kiti chako cha ufalme ukihukumu kwa haki.+
ג [Gimel]
5 Umekemea mataifa+ na kuharibu waovu,Na hivyo unafuta jina lao milele na milele.
6 Adui ameharibiwa milele;Ulingoa miji yao,Na kumbukumbu lote kuwahusu litapotea.+
ה [He]
7 Lakini Yehova amekaa akiwa mufalme milele;+Amefanya imara kabisa kiti chake cha ufalme kwa ajili ya haki.+
8 Atahukumu kwa haki dunia yenye kuikaliwa na watu;*+Atafanya maamuzi ya hukumu yenye haki kwa ajili ya mataifa.+
ו [Waw]
9 Yehova atakuwa kimbilio salama* kwa ajili ya wale wenye kukandamizwa,+Kimbilio salama katika nyakati za taabu.+
10 Wale wenye kujua jina lako watakutegemea wewe;+Hautaacha hata kidogo wale wenye kukutafuta, Ee Yehova.+
ז [Zayin]
11 Mumuimbie Yehova sifa, mwenye kukaa Sayuni;Mujulishe matendo yake kati ya vikundi vya watu.+
12 Kwa maana Ule mwenye analipiza kisasi kwa ajili ya damu yao anawakumbuka;+Hatasahau kilio cha wenye kuteseka.+
ח [Heth]
13 Unionyeshe wema, Ee Yehova; angalia namna wale wenye kunichukia wananitesa,Wewe mwenye kuniinua kutoka katika milango mikubwa ya kifo,+
14 Ili nitangaze katika milango mikubwa ya binti ya Sayuni+ matendo yako yenye kustahili sifa,Na kushangilia katika matendo yako ya wokovu.+
ט [Teth]
15 Mataifa yamezama chini katika shimo lenye walichimba;Muguu wao wenyewe umenaswa katika wavu wenye* walificha.+
16 Yehova anajulikana kupitia hukumu zenye anafanya.+
Muovu amenaswa katika kazi za mikono yake mwenyewe.+
Higayoni.* (Sela)
י [Yod]
17 Waovu watarudia nyuma kuelekea Kaburi,*Mataifa yote yenye kumusahau Mungu.
18 Lakini maskini hawatasahauliwa sikuzote;+Wala tumaini la wapole halitapotea hata kidogo.+
כ [Kaph]
19 Simama, Ee Yehova! Usiache mwanadamu mwenye anaweza kufa ashinde.
Acha mataifa yahukumiwe mbele yako.+
20 Uwapige kwa woga, Ee Yehova,+Mataifa yajue kwamba wao ni wanadamu tu wenye wanaweza kufa. (Sela)
Maelezo ya Chini
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “Nitapigia jina lako muziki.”
^ Ao “inchi yenye kuzaa.”
^ Ao “mahali salama pa juu.”
^ Ao “makila yenye.”
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.