Zaburi 141:1-10
Muziki wa Daudi.
141 Ee Yehova, ninakuitia.+
Kuja haraka unisaidie.+
Sikiliza wakati ninakuita.+
2 Sala yangu ikuwe kama uvumba+ wenye kutayarishwa mbele yako,+Mikono yangu yenye kuinuliwa ikuwe kama toleo la nafaka la mangaribi.+
3 Weka mulinzi kwa ajili ya kinywa changu, Ee Yehova,Weka ulinzi kwenye mulango wa midomo yangu.+
4 Usiache moyo wangu uelekee kwenye jambo lolote la mubaya,+Ili nisishiriki katika matendo maovu pamoja na watu waovu;Nisikule hata kidogo vyakula vyao vitamu.
5 Kama mwenye haki ananipiga, hilo litakuwa tendo la upendo mushikamanifu;+Kama ananikaripia, hilo litakuwa kama mafuta kwenye kichwa changu,+Yenye kichwa changu hakitakataa hata kidogo.+
Sala yangu itaendelea hata wakati wa misiba yao.
6 Hata kama waamuzi wao wanatupwa chini kutoka kwenye muteremuko mukali,Watu watasikiliza maneno yangu, kwa maana ni yenye kupendeza.
7 Kama vile wakati mutu analima na kuvunja-vunja udongo,Ni vile mifupa yetu imesambazwa kwenye kinywa cha Kaburi.*
8 Lakini macho yangu yanakuangalia, Ee Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova.+
Nimekukimbilia.
Usiondoe uzima wangu.*
9 Unilinde kutokana na mataya* ya mutego wenye wamenitegea,Kutokana na mitego ya watenda-maovu.
10 Waovu wataanguka wote pamoja ndani ya nyavu zao* wenyewe+Lakini mimi nitapita karibu nayo kwa usalama.
Maelezo ya Chini
^ Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “Usimwange nafsi yangu.”
^ Mataya ni mifupa ya kinywa yenye kubeba meno.
^ Ao “makila yao.”