ULIZO LA 14
Namna Gani Unaweza Kutumia Mali Yako?
“Mwenye anapenda kujifurahisha atakuwa maskini; mwenye anapenda divai na mafuta hatakuwa tajiri.”
“Mukopaji ni mutumwa wa mukopeshaji.”
“Ni nani kati yenu mwenye akitaka kujenga munara hakae kwanza na kuhesabia garama, ili aone kama iko na vitu vya kutosha ili kuumaliza? Kama hafanye vile, anaweza kuweka musingi lakini anashindwa kumaliza munara, na wale wenye kumuangalia wataanza kumuchekelea, na kusema: ‘Mutu huyu alianza kujenga lakini hakuweza kumaliza.’”
“Wakati walikuwa wamekula na kushiba, akaambia wanafunzi wake: ‘Mukusanye pamoja vipande vyenye vilibakia, ili kitu chochote kisipotee.’”