Zaburi 129:1-8
-
Alishambuliwa lakini hakushindwa
-
Wenye kuchukia Sayuni wanapatishwa haya (5)
-
Wimbo wa Safari za Kupanda.
129 “Wamenishambulia kila wakati tangu ujana wangu”+—Israeli aseme sasa—
2 “Wamenishambulia kila wakati tangu ujana wangu;+Lakini hawajanishinda.+
3 Walimaji wamelima kwenye mugongo wangu;+Wamerefusha mifereji yao.”
4 Lakini Yehova ni mwenye haki;+Amekata-kata kamba za waovu.+
5 Watapatishwa haya na kukimbia kwa sababu ya aibu,Wale wote wenye kuchukia Sayuni.+
6 Watakuwa kama majani kwenye sehemu za juu za nyumbaYenye yanakauka mbele yangolewe,
7 Yenye hayawezi kujaa katika mukono wa muvunajiWala katika mikono ya ule mwenye kukusanya mafungu ya mbegu.
8 Wale wenye kupita karibu hawatasema:
“Baraka ya Yehova ikuwe juu yenu;Tunawabariki katika jina la Yehova.”