Zaburi 67:1-7

  • Miisho ya dunia itamuogopa Mungu

    • Njia ya Mungu itajulikana (2)

    • ‘Acha vikundi vyote vya watu vimusifu Mungu’ (3,5)

    • “Mungu atatubariki” (6, 7)

Kwa kiongozi; iimbwe kwa vyombovya kamba. Muziki. Wimbo. 67  Mungu atatuonyesha wema na kutubariki;Atafanya uso wake utuangazie+ (Sela)  2  Ili njia yako ijulikane katika dunia yote,+Matendo yako ya wokovu kati ya mataifa yote.+  3  Vikundi vya watu vitakusifu, Ee Mungu;Vikundi vyote vya watu vikusifu.  4  Mataifa yashangilie na kupiga vigelegele vya shangwe,+Kwa maana utahukumu vikundi vya watu kwa haki.+ Utaongoza mataifa ya dunia. (Sela)  5  Vikundi vya watu vikusifu, Ee Mungu;Vikundi vyote vya watu vikusifu.  6  Dunia itatoa mazao yake;+Mungu, Mungu wetu, atatubariki.+  7  Mungu atatubariki,Na miisho yote ya dunia itamuogopa* yeye.+

Maelezo ya Chini

Ao “itamuheshimia.”