Zaburi 5:1-12
Kwa kiongozi wa Nehiloti.*
Muziki wa Daudi.
5 Sikiliza maneno yangu, Ee Yehova;+Sikiliza kwa uangalifu kilio changu cha maumivu.
2 Sikiliza kilio changu cha kuomba musaada,Ee Mufalme wangu na Mungu wangu, kwa sababu ninasali kwako.
3 Ee Yehova, utasikia sauti yangu asubui;+Asubui nitakuelezea mahangaiko yangu+ na kungojea kwa hamu.
4 Kwa maana wewe hauko Mungu mwenye anafurahia uovu;+Hakuna mutu yeyote mubaya mwenye anaweza kukaa pamoja na wewe.+
5 Hakuna mutu yeyote mwenye kiburi mwenye anaweza kusimama mbele yako.
Unachukia wale wote wenye kutenda maovu;+
6 Utaharibu wale wenye kusema uongo.+
Yehova anachukia watu wenye jeuri na wadanganyifu.*+
7 Lakini nitaingia katika nyumba yako+ kwa sababu ya upendo wako mwingi mushikamanifu;+Nitainama chini kuelekea hekalu lako takatifu* nikiwa na woga wenye heshima kukuelekea.+
8 Uniongoze, Ee Yehova, katika haki yako kwa sababu ya maadui wangu;Fanya njia yako ikuwe wazi kwangu.+
9 Kwa maana hakuna kitu chochote chenye wanasema chenye kinaweza kutumainiwa;Ndani yao hamuna kitu chochote isipokuwa tu nia mubaya.
Koo yao ni kaburi lenye kuwa wazi;Wanasifu-sifu kwa ulimi wao.*+
10 Lakini Mungu atawatangaza kuwa na hatia;Mipango yao mibaya itafanya waanguke.+
Wafukuzwe kwa sababu ya makosa yao mengi,Kwa maana wamekuasi wewe.
11 Lakini wale wote wenye kukukimbilia watashangilia;+Watapiga vigelegele vya shangwe sikuzote.
Na utaweka kizuizi ili wasifikiwe,Na wale wenye kupenda jina lako watashangilia katika wewe.
12 Kwa maana utamubariki mutu yeyote mwenye haki, Ee Yehova;Utawazunguka kwa kuwakubali kama vile kwa ngao kubwa.+
Maelezo ya Chini
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “mutu mwenye kumwanga damu na ambaye ni mudanganyifu.”
^ Ao “patakatifu pako.”
^ Ao “Wanatumia ulimi laini.”

