Zaburi 5:1-12

  • Yehova ni kimbilio la mwenye haki

    • Mungu anachukia uovu (4, 5)

    • ‘Uniongoze katika haki yako’ (8)

Kwa kiongozi wa Nehiloti.* Muziki wa Daudi. 5  Sikiliza maneno yangu, Ee Yehova;+Sikiliza kwa uangalifu kilio changu cha maumivu.  2  Sikiliza kilio changu cha kuomba musaada,Ee Mufalme wangu na Mungu wangu, kwa sababu ninasali kwako.  3  Ee Yehova, utasikia sauti yangu asubui;+Asubui nitakuelezea mahangaiko yangu+ na kungojea kwa hamu.  4  Kwa maana wewe hauko Mungu mwenye anafurahia uovu;+Hakuna mutu yeyote mubaya mwenye anaweza kukaa pamoja na wewe.+  5  Hakuna mutu yeyote mwenye kiburi mwenye anaweza kusimama mbele yako. Unachukia wale wote wenye kutenda maovu;+  6  Utaharibu wale wenye kusema uongo.+ Yehova anachukia watu wenye jeuri na wadanganyifu.*+  7  Lakini nitaingia katika nyumba yako+ kwa sababu ya upendo wako mwingi mushikamanifu;+Nitainama chini kuelekea hekalu lako takatifu* nikiwa na woga wenye heshima kukuelekea.+  8  Uniongoze, Ee Yehova, katika haki yako kwa sababu ya maadui wangu;Fanya njia yako ikuwe wazi kwangu.+  9  Kwa maana hakuna kitu chochote chenye wanasema chenye kinaweza kutumainiwa;Ndani yao hamuna kitu chochote isipokuwa tu nia mubaya. Koo yao ni kaburi lenye kuwa wazi;Wanasifu-sifu kwa ulimi wao.*+ 10  Lakini Mungu atawatangaza kuwa na hatia;Mipango yao mibaya itafanya waanguke.+ Wafukuzwe kwa sababu ya makosa yao mengi,Kwa maana wamekuasi wewe. 11  Lakini wale wote wenye kukukimbilia watashangilia;+Watapiga vigelegele vya shangwe sikuzote. Na utaweka kizuizi ili wasifikiwe,Na wale wenye kupenda jina lako watashangilia katika wewe. 12  Kwa maana utamubariki mutu yeyote mwenye haki, Ee Yehova;Utawazunguka kwa kuwakubali kama vile kwa ngao kubwa.+

Maelezo ya Chini

Ao “mutu mwenye kumwanga damu na ambaye ni mudanganyifu.”
Ao “patakatifu pako.”
Ao “Wanatumia ulimi laini.”