Zaburi 71:1-24
71 Nimekukimbilia wewe, Ee Yehova.
Usiache nipatishwe haya hata kidogo.+
2 Katika haki yako uniokoe na kunikomboa.
Unitegee sikio lako* na kuniokoa.+
3 Ukuwe ngome ya mwamba kwa ajili yanguKwenye ninaweza kuingia sikuzote.
Toa amri ya kuniokoa,Kwa maana wewe ni mwamba wangu na ngome yangu.+
4 Ee Mungu wangu, uniokoe kutoka katika mukono wa muovu,+Kutoka katika kushikwa na mukandamizaji mwenye hana haki.
5 Kwa maana wewe ni tumaini langu, Ee Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi, Yehova;Nimekutegemea wewe* tangu ujana wangu.+
6 Nimekutegemea tangu kuzaliwa kwangu;Wewe ndiye ulinitosha katika tumbo la uzazi la mama yangu.+
Ninakusifu kila wakati.
7 Nimekuwa kama muujiza kwa watu wengi,Lakini wewe ni kimbilio lenye nguvu.
8 Kinywa changu kimejaa sifa zako;+Muchana wote ninasimulia kuhusu utukufu wako.
9 Usinitupe wakati wa uzee;+Usiniache wakati nguvu zangu zinaisha.+
10 Maadui wangu wanasema mubaya juu yangu,Na wale wenye kutafuta kuondoa uzima wangu* wanafanya pamoja mupango mubaya,+
11 Kwa kusema: “Mungu amemuacha.
Mumufuatilie na kumukamata, kwa maana hakuna mutu wa kumuokoa.”+
12 Ee Mungu, usiendelee kukaa mbali na mimi.
Ee Mungu wangu, fanya haraka ili unisaidie.+
13 Acha wale wenye kunipinga*Wapatishwe haya na kuangamia.+
Acha wale wenye kutafuta musiba wanguWafunikwe haya na aibu.+
14 Lakini mimi, nitaendelea kungojea;Nitakusifu hata zaidi.
15 Kinywa changu kitasimulia haki yako,+Muchana wote kitasimulia matendo yako ya wokovu,Hata kama ni mengi sana kwangu kuelewa.*+
16 Nitakuja na kutangaza matendo yako yenye nguvu,Ee Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova;Nitatangaza haki yako, yako tu.
17 Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu,+Na mupaka sasa ninaendelea kutangaza kazi zako za ajabu.+
18 Ee Mungu, hata wakati nitazeeka na kuwa na imvi, usiniache.+
Acha niambie kizazi chenye kitafuata kuhusu nguvu zako*Na kuambia wale wote wenye watakuja kuhusu uwezo wako.+
19 Haki yako, Ee Mungu, inafika kwenye nafasi za juu;+Umetenda mambo makubwa;Ee Mungu, ni nani mwenye kuwa kama wewe?+
20 Hata kama umenifanya nipate taabu nyingi na misiba mingi,+Unipatie tena uzima;Uniinue kutoka katika sehemu za chini kabisa za* dunia.+
21 Ongeza ukubwa wanguNa unizunguke na kunifariji.
22 Kisha nitakusifu kwa chombo cha kambaKwa sababu ya uaminifu wako, Ee Mungu wangu.+
Nitaimba sifa zako* kwa kinubi,Ee Mutakatifu wa Israeli.
23 Midomo yangu itapiga vigelegele vya shangwe wakati ninakuimbia sifa,+Kwa maana umeokoa uzima wangu.*+
24 Ulimi wangu utaongea* muchana wote kuhusu haki yako,+Kwa maana wale wenye kutafuta kuniharibu watapatishwa haya na kufezeheshwa.+
Maelezo ya Chini
^ Ao “Uiname chini na unisikilize.”
^ Ao “Wewe ni tegemeo langu.”
^ Ao “kutafuta nafsi yangu.”
^ Ao “kupinga nafsi yangu.”
^ Ao “kuhesabia.”
^ Tnn., “mukono wako.”
^ Ao “maji yenye kuenda chini sana ya.”
^ Ao “Nitakupigia muziki.”
^ Ao “umekomboa nafsi yangu.”
^ Ao “utatafakari; utafikiri sana.”