Zaburi 82:1-8

  • Wanaombwa wahukumu kwa haki

    • Mungu anahukumu kati ya “miungu” (1)

    • “Mutetee mutu wa hali ya chini” (3)

    • “Ninyi ni miungu” (6)

Muziki wa Asafu.+ 82  Mungu anakamata nafasi yake katika mukusanyiko wa kimungu;*+Anahukumu katikati ya miungu:*+  2  “Mutaendelea kuhukumu bila haki mupaka wakati gani+Na kupendelea waovu?+ (Sela)  3  Mutetee* mutu wa hali ya chini na mwenye hana baba.+ Mutendee kwa haki mutu mwenye hana uwezo na maskini.+  4  Mumuokoe mutu wa hali ya chini na maskini;Muwaokoe katika mukono wa muovu.”  5  Hawajue wala hawaelewe;+Wanatembea huku na huku katika giza;Misingi yote ya dunia inatikiswa.+  6  “Mimi nimesema, ‘Ninyi ni miungu,*+Ninyi wote muko wana wa Mwenye Kuwa Juu Zaidi.  7  Lakini mutakufa kama vile wanadamu wanakufa;+Na mutaanguka kama vile mukubwa mwingine yeyote!’”+  8  Simama, Ee Mungu, na uhukumu dunia,+Kwa maana mataifa yote ni yako.

Maelezo ya Chini

Ao “katika mukusanyiko wa Mungu.”
Ao “wenye kuwa kama Mungu.”
Ao “Muhukumu kwa ajili ya.”
Ao “muko kama Mungu.”