Zaburi 76:1-12

  • Mungu anashinda maadui wa Sayuni

    • Mungu anaokoa wapole (9)

    • Maadui wenye kiburi watanyenyekezwa (12)

Kwa kiongozi; iimbwe kwa vyombo vya kamba. Muziki wa Asafu.+ Wimbo. 76  Mungu anajulikana katika Yuda;+Jina lake ni kubwa katika Israeli.+  2  Kibanda chake kiko katika Salemu,+Na makao yake yako katika Sayuni.+  3  Kule alivunja mishale ya upinde yenye kuwaka,Ngao na upanga na silaha za vita.+ (Sela)  4  Unangaa sana;*Uko na utukufu kuliko milima ya mawindo.  5  Vitu vya watu wenye moyo hodari vimenyanganywa.+ Wamelala usingizi;Wapiganaji-vita wote hawakukuwa na uwezo.+  6  Kwa sababu ya kemeo lako, Ee Mungu wa Yakobo,Muendesha-gari na farasi pia wamelala usingizi muzito.+  7  Wewe peke yako ndiye mwenye kuogopesha sana.+ Na ni nani anaweza kuvumilia kasirani yako kali?+  8  Kutoka mbinguni ulitangaza hukumu;+Dunia iliogopa na kunyamaza+  9  Wakati Mungu alisimama ili kuleta hukumu,Ili kuokoa wapole wote wa dunia.+ (Sela) 10  Kwa maana kasirani kali ya mwanadamu itakuletea sifa;+Na utajipamba kwa mabaki ya kasirani yao kali. 11  Muweke naziri zenu kwa Yehova Mungu wenu na kuzitimiza,+Acha wote wenye kumuzunguka walete zawadi yao kwa woga.+ 12  Atanyenyekeza kiburi* cha viongozi;Yeye anaogopesha wafalme wa dunia.

Maelezo ya Chini

Ao “Umefunikwa mwangaza.”
Tnn., “roho.”