Zaburi 76:1-12
Kwa kiongozi; iimbwe kwa vyombo vya kamba. Muziki wa Asafu.+ Wimbo.
76 Mungu anajulikana katika Yuda;+
Jina lake ni kubwa katika Israeli.+
2 Kibanda chake kiko katika Salemu,+
Na makao yake yako katika Sayuni.+
3 Kule alivunja mishale ya upinde yenye kuwaka,
Ngao na upanga na silaha za vita.+ (Sela)
4 Unangaa sana;*
Uko na utukufu kuliko milima ya mawindo.
5 Vitu vya watu wenye moyo hodari vimenyanganywa.+
Wamelala usingizi;
Wapiganaji-vita wote hawakukuwa na uwezo.+
6 Kwa sababu ya kemeo lako, Ee Mungu wa Yakobo,
Muendesha-gari na farasi pia wamelala usingizi muzito.+
7 Wewe peke yako ndiye mwenye kuogopesha sana.+
Na ni nani anaweza kuvumilia kasirani yako kali?+
8 Kutoka mbinguni ulitangaza hukumu;+
Dunia iliogopa na kunyamaza+
9 Wakati Mungu alisimama ili kuleta hukumu,
Ili kuokoa wapole wote wa dunia.+ (Sela)
10 Kwa maana kasirani kali ya mwanadamu itakuletea sifa;+
Na utajipamba kwa mabaki ya kasirani yao kali.
11 Muweke naziri zenu kwa Yehova Mungu wenu na kuzitimiza,+
Acha wote wenye kumuzunguka walete zawadi yao kwa woga.+
12 Atanyenyekeza kiburi* cha viongozi;
Yeye anaogopesha wafalme wa dunia.