Zaburi 76:1-12

  • Mungu anashinda maadui wa Sayuni

    • Mungu anaokoa wapole (9)

    • Maadui wenye kiburi watanyenyekezwa (12)

Kwa kiongozi; iimbwe kwa vyombo vya kamba. Muziki wa Asafu.+ Wimbo. 76  Mungu anajulikana katika Yuda;+ Jina lake ni kubwa katika Israeli.+   Kibanda chake kiko katika Salemu,+ Na makao yake yako katika Sayuni.+   Kule alivunja mishale ya upinde yenye kuwaka, Ngao na upanga na silaha za vita.+ (Sela)   Unangaa sana;* Uko na utukufu kuliko milima ya mawindo.   Vitu vya watu wenye moyo hodari vimenyanganywa.+ Wamelala usingizi; Wapiganaji-vita wote hawakukuwa na uwezo.+   Kwa sababu ya kemeo lako, Ee Mungu wa Yakobo, Muendesha-gari na farasi pia wamelala usingizi muzito.+   Wewe peke yako ndiye mwenye kuogopesha sana.+ Na ni nani anaweza kuvumilia kasirani yako kali?+   Kutoka mbinguni ulitangaza hukumu;+ Dunia iliogopa na kunyamaza+   Wakati Mungu alisimama ili kuleta hukumu, Ili kuokoa wapole wote wa dunia.+ (Sela) 10  Kwa maana kasirani kali ya mwanadamu itakuletea sifa;+ Na utajipamba kwa mabaki ya kasirani yao kali. 11  Muweke naziri zenu kwa Yehova Mungu wenu na kuzitimiza,+ Acha wote wenye kumuzunguka walete zawadi yao kwa woga.+ 12  Atanyenyekeza kiburi* cha viongozi; Yeye anaogopesha wafalme wa dunia.

Maelezo ya Chini

Ao “Umefunikwa mwangaza.”
Tnn., “roho.”