Zaburi 65:1-13

  • Mungu anatunza dunia

    • “Musikiaji wa sala” (2)

    • “Mwenye furaha ni ule mwenye unachagua” (4)

    • Wema mwingi wa Mungu (11)

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi. Wimbo. 65  Sifa inakungojea, Ee Mungu, katika Sayuni;+Tutatimiza naziri zenye tumeweka kwako.+   Ee Musikiaji wa sala, watu wa namna zote* watakuendea.+   Zambi zangu zimenilemea,+Lakini unafunika makosa yetu.+   Mwenye furaha ni ule mwenye unachagua na kumuleta karibu+Ili akae katika viwanja vyako.+ Tutatosheka na wema wa nyumba yako,Hekalu lako takatifu.*+   Utatujibu kwa matendo ya haki yenye kuogopesha sana,+Ee Mungu wa wokovu wetu;Wewe ndiye Tegemeo la miisho yote ya dunia+Na la wale wenye kuwa mbali ngambo ya bahari.   Ulifanya* milima ikuwe imara kabisa kwa nguvu zako;Umevaa* uwezo.+   Unatuliza* bahari zenye kuchafuka,+Kishindo cha mawimbi yake na musukosuko wa mataifa.+   Wakaaji wa sehemu za mbali wataogopeshwa na alama zako;+Utafanya wale wenye kuishi mahali jua linatokea mupaka mahali jua linashukia wapige vigelegele vya shangwe.   Unatunza dunia,Unaifanya izae kwa wingi* na kuifanya ikuwe tajiri sana.+ Muto mudogo kutoka kwa Mungu umejaa maji;Unawapatia nafaka,+Kwa maana ni vile ulitayarisha dunia. 10  Unajaza maji katika mifereji yake na kusawazisha udongo wake wenye umelimwa;*Unaifanya kuwa laini kwa matone ya mvua; unabariki mimea yake.+ 11  Unavalisha mwaka taji la wema wako;Njia zako zinajaa wingi wa vitu.*+ 12  Malisho yanaendelea kujaa sana,*+Na vilima vimevalishwa shangwe.+ 13  Malisho yamefunikwa na makundi,Na mabonde* yamefunikwa na nafaka.+ Yanapiga vigelegele vya ushindi, ndiyo, yanaimba.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “watu wote wenye mwili.”
Ao “Patakatifu pako.”
Tnn., “Alifanya.”
Tnn., “Amevaa.”
Tnn., “Anatuliza.”
Tnn., “ijae sana.”
Ao “matuta yake.”
Tnn., “yanaangusha matone-matone ya mafuta.”
Tnn., “kuangusha matone-matone.”
Ao “maeneo tambarare ya chini.”