Zaburi 24:1-10

  • Mufalme mwenye utukufu anaingia katika milango mikubwa

    • ‘Dunia ni ya Yehova’ (1)

Ya Daudi. Muziki. 24  Dunia na vyote vyenye kuwa ndani yake ni vya Yehova,+Inchi yenye kuzaa na wale wenye kukaa juu yake.  2  Kwa maana ameiweka imara kabisa juu ya bahari+Na kuiweka imara kabisa juu ya mito.  3  Ni nani anaweza kupanda mulima wa Yehova,+Na ni nani anaweza kusimama mahali pake patakatifu?  4  Mutu yeyote mwenye mikono yenye haina kosa na mwenye moyo safi,+Mwenye hajaapa kiapo cha uongo kwa uzima Wangu,*Wala kuapa kwa udanganyifu.+  5  Atapokea baraka kutoka kwa Yehova+Na haki kutoka kwa Mungu wake wa wokovu.+  6  Hiki ni kizazi cha wale wenye kumutafuta,Cha wale wenye kutafuta uso wako, Ee Mungu wa Yakobo. (Sela)  7  Muinue vichwa vyenu, ninyi milango mikubwa;+Mufunguke,* ninyi miingilio ya zamani,Ili Mufalme mwenye utukufu aingie!+  8  Mufalme huyu mwenye utukufu ni nani? Yehova, mwenye nguvu na uwezo,+Yehova, mwenye uwezo katika vita.+  9  Muinue vichwa vyenu, ninyi milango mikubwa;+Mufunguke, ninyi miingilio ya zamani,Ili Mufalme mwenye utukufu aingie! 10  Yeye ni nani, huyo Mufalme mwenye utukufu? Yehova wa majeshi​—⁠yeye ndiye Mufalme mwenye utukufu.+ (Sela)

Maelezo ya Chini

Ao “nafsi Yangu,” inamaanisha uzima wa Yehova wenye mutu anaapa kwa huo.
Ao “Musimame.”