Zaburi 97:1-12
97 Yehova amekuwa Mufalme!+
Dunia ifurahi.+
Visiwa vingi vishangilie.+
2 Mawingu na giza nzito vinamuzunguka pande zote;+Uadilifu* na haki ndio musingi wa kiti chake cha ufalme.+
3 Moto unamutangulia+Na kuteketeza wapinzani wake kila upande.+
4 Umeme wake wa radi unaangazia inchi;Dunia inauona na kutetemeka.+
5 Milima inayeyuka kama nta* mbele ya Yehova,+Mbele ya Bwana wa dunia yote.
6 Mbingu zinatangaza haki yake,Na vikundi vyote vya watu vinaona utukufu wake.+
7 Acha wale wote wenye kutumikia sanamu yoyote ya kuchongwa wapatishwe haya,+Wale wenye kujisifu kuhusu miungu yao yenye haina mafaa yoyote.+
Mumuinamie,* ninyi miungu yote.+
8 Sayuni inasikia na kushangilia;+Miji ya Yuda imefurahi*Kwa sababu ya hukumu zako, Ee Yehova.+
9 Kwa maana wewe, Ee Yehova, ndiye Mwenye Kuwa Juu Zaidi, juu ya dunia yote;Umeinuliwa juu zaidi kuliko miungu mingine yote.+
10 Enyi wenye kumupenda Yehova, muchukie mambo ya mubaya.+
Analinda uzima wa* washikamanifu wake;+Anawaokoa katika mukono wa* waovu.+
11 Mwangaza umeangazia wenye haki+Na shangwe imeangazia wale wenye kuwa wanyoofu katika moyo.
12 Mushangilie katika Yehova, ninyi wenye haki,Na mushukuru jina lake takatifu.*

