Zaburi 61:1-8

  • Mungu ni munara wenye nguvu juu ya maadui

    • “Nitakuwa mugeni katika hema yako” (4)

Kwa kiongozi; iimbwe kwavyombo vya kamba. Ya Daudi. 61  Ee Mungu, sikia kilio changu cha kuomba musaada. Sikiliza sala yangu.+  2  Nitakulilia kwa sauti kutoka kwenye miisho ya duniaWakati moyo wangu umepoteza tumaini.*+ Uniongoze kwenye mwamba wenye kuwa juu kuliko mimi.+  3  Kwa maana wewe ni kimbilio langu,Munara wenye nguvu wenye unanilinda na adui.+  4  Nitakuwa mugeni katika hema yako milele;+Nitakimbilia katika kivuli cha mabawa yako.+ (Sela)  5  Kwa maana wewe, Ee Mungu, umesikia naziri zangu. Umenipatia uriti wa wale wenye kuogopa jina lako.+  6  Utaongeza siku kwenye maisha ya* mufalme,+Na miaka yake itakuwa kuanzia kizazi mupaka kizazi.  7  Atakaa akiwa mufalme* milele mbele ya Mungu;+Umupatie* upendo wako mushikamanifu na uaminifu, ili vimulinde.+  8  Kisha nitaimbia jina lako sifa* milele,+Wakati nitakuwa ninatimiza naziri zangu siku kwa siku.+

Maelezo ya Chini

Ao “unakuwa zaifu.”
Tnn., “siku za.”
Ao “atakaa.”
Ao “Umugawie.”
Ao “nitapigia jina lako muziki.”