Zaburi 61:1-8
-
Mungu ni munara wenye nguvu juu ya maadui
-
“Nitakuwa mugeni katika hema yako” (4)
-
Kwa kiongozi; iimbwe kwavyombo vya kamba. Ya Daudi.
61 Ee Mungu, sikia kilio changu cha kuomba musaada.
Sikiliza sala yangu.+
2 Nitakulilia kwa sauti kutoka kwenye miisho ya dunia
Wakati moyo wangu umepoteza tumanini.*+
Uniongoze kwenye mwamba wenye kuwa juu kuliko mimi.+
3 Kwa maana wewe ni kimbilio langu,
Munara wenye nguvu wenye unanilinda na adui.+
4 Nitakuwa mugeni katika hema yako milele;+
Nitakimbilia katika kivuli cha mabawa yako.+ (Sela)
5 Kwa maana wewe, Ee Mungu, umesikia naziri zangu.
Umenipatia uriti wa wale wenye kuogopa jina lako.+
6 Utaongeza siku kwenye maisha ya* mufalme,+
Na miaka yake itakuwa kuanzia kizazi mupaka kizazi.
7 Atakaa akiwa mufalme* milele mbele ya Mungu;+
Umupatie* upendo wako mushikamanifu na uaminifu, ili vimulinde.+
8 Kisha nitaimbia jina lako sifa* milele,+
Wakati nitakuwa ninatimiza naziri zangu siku kwa siku.+
Maelezo ya Chini
^ Ao “unakuwa zaifu.”
^ Tnn., “siku za.”
^ Ao “atakaa.”
^ Ao “Umugawie.”
^ Ao “nitapigia jina lako muziki.”