Zaburi 57:1-11
Kwa kiongozi; imepatanishwa na “Usiharibu.” Ya Daudi. Miktamu.* Wakati alimukimbia Sauli na kuingia katika pango.+
57 Unionyeshe wema, Ee Mungu, unionyeshe wema,Kwa maana ninakukimbilia,*+Na ninakimbilia kivuli cha mabawa yako mupaka magumu yangu yapite.+
2 Ninamuita Mungu Mwenye Kuwa Juu Zaidi,Mungu wa kweli, mwenye anamaliza magumu hayo kwa ajili yangu.
3 Atatuma musaada kutoka mbinguni na kuniokoa.+
Atamuvuruga ule mwenye anataka kuniuma. (Sela)
Mungu atatuma upendo wake mushikamanifu na uaminifu wake.+
4 Nimezungukwa* na simba;+Nimelazimika kulala kati ya watu wenye wanataka kunimeza,Wenye meno yao ni mikuki na mishaleNa wenye ulimi wao ni upanga mukali.+
5 Uinuliwe juu ya mbingu, Ee Mungu;Utukufu wako ukuwe juu ya dunia yote.+
6 Wametayarisha wavu* ili kunasa miguu yangu;+Nimeinama* chini kwa sababu ya taabu.+
Wamechimba shimo mbele yangu,Lakini wao wenyewe wameanguka ndani.+ (Sela)
7 Moyo wangu uko imara, Ee Mungu,+Moyo wangu uko imara.
Nitaimba na kupiga muziki.
8 Amuka, utukufu wangu.
Amuka, Ee chombo cha kamba; na wewe pia, Ee kinubi.
Nitaamusha mapambazuko.*+
9 Nitakusifu kati ya vikundi vya watu, Ee Yehova;+Nitakuimbia sifa* kati ya mataifa.+
10 Kwa maana upendo wako mushikamanifu ni mwingi, uko juu kama mbingu,+Na uaminifu wako, unafika mupaka kwenye anga.
11 Uinuliwe juu ya mbingu, Ee Mungu;Utukufu wako ukuwe juu ya dunia yote.+
Maelezo ya Chini
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “nafsi yangu inakukimbilia.”
^ Ao “Nafsi yangu imezungukwa.”
^ Ao “Nafsi yangu imeinama.”
^ Ao “makila.”
^ Mapambazuko ni wakati mwangaza wa asubui unaanza kutokea.
^ Ao “Nitakupigia muziki.”