Zaburi 57:1-11

  • Sala ya kuomba rehema

    • Kukimbilia chini ya mabawa ya Mungu (1)

    • Maadui wanaanguka katika mutego wao wenyewe (6)

Kwa kiongozi; imepatanishwa na “Usiharibu.” Ya Daudi. Miktamu.* Wakati alimukimbia Sauli na kuingia katika pango.+ 57  Unionyeshe wema, Ee Mungu, unionyeshe wema,Kwa maana ninakukimbilia,*+Na ninakimbilia kivuli cha mabawa yako mupaka magumu yangu yapite.+  2  Ninamuita Mungu Mwenye Kuwa Juu Zaidi,Mungu wa kweli, mwenye anamaliza magumu hayo kwa ajili yangu.  3  Atatuma musaada kutoka mbinguni na kuniokoa.+ Atamuvuruga ule mwenye anataka kuniuma. (Sela) Mungu atatuma upendo wake mushikamanifu na uaminifu wake.+  4  Nimezungukwa* na simba;+Nimelazimika kulala kati ya watu wenye wanataka kunimeza,Wenye meno yao ni mikuki na mishaleNa wenye ulimi wao ni upanga mukali.+  5  Uinuliwe juu ya mbingu, Ee Mungu;Utukufu wako ukuwe juu ya dunia yote.+  6  Wametayarisha wavu* ili kunasa miguu yangu;+Nimeinama* chini kwa sababu ya taabu.+ Wamechimba shimo mbele yangu,Lakini wao wenyewe wameanguka ndani.+ (Sela)  7  Moyo wangu uko imara, Ee Mungu,+Moyo wangu uko imara. Nitaimba na kupiga muziki.  8  Amuka, utukufu wangu. Amuka, Ee chombo cha kamba; na wewe pia, Ee kinubi. Nitaamusha mapambazuko.*+  9  Nitakusifu kati ya vikundi vya watu, Ee Yehova;+Nitakuimbia sifa* kati ya mataifa.+ 10  Kwa maana upendo wako mushikamanifu ni mwingi, uko juu kama mbingu,+Na uaminifu wako, unafika mupaka kwenye anga. 11  Uinuliwe juu ya mbingu, Ee Mungu;Utukufu wako ukuwe juu ya dunia yote.+

Maelezo ya Chini

Ao “nafsi yangu inakukimbilia.”
Ao “Nafsi yangu imezungukwa.”
Ao “Nafsi yangu imeinama.”
Ao “makila.”
Mapambazuko ni wakati mwangaza wa asubui unaanza kutokea.
Ao “Nitakupigia muziki.”