Zaburi 128:1-6
Wimbo wa Safari za Kupanda.
128 Mwenye furaha ni kila mutu mwenye anamuogopa Yehova,+
Mwenye anatembea katika njia Zake.+
2 Utakula vitu vyenye mukono wako ulifanya kazi ya nguvu ili kuvipata.
Utakuwa na furaha na kufurahia mafanikio.+
3 Bibi yako atakuwa kama muzabibu wenye kuzaa matunda mengi ndani ya nyumba yako;+
Wana wako watakuwa kama machipukizi ya muzeituni kuzunguka meza yako.
4 Angalia! Ni vile mwanaume mwenye kumuogopa Yehova
Atabarikiwa.+
5 Yehova atakubariki kutoka Sayuni.
Na uone Yerusalemu ikisitawi sikuzote za maisha yako+
6 Na uone wana wa wana wako.
Amani ikuwe juu ya Israeli.