Zaburi 26:1-12
Ya Daudi.
26 Unihukumu, Ee Yehova, kwa maana nimetembea katika uaminifu-mushikamanifu wangu;+Nimemutegemea Yehova bila kuyumba-yumba.+
2 Unichunguze, Ee Yehova, na unijaribu;Usafishe mawazo yangu ya ndani kabisa* na pia moyo wangu.+
3 Kwa maana upendo wako mushikamanifu uko mbele yangu sikuzote,Na ninatembea katika kweli yako.+
4 Sishirikiane* na watu wadanganyifu,+Na ninaepuka wale wenye kuficha namna wako.*
5 Ninachukia kuwa pamoja na waovu,+Na ninakataa kushirikiana* na waovu.+
6 Nitanawa mikono yangu katika kukosa kuwa na hatia,Na nitatembea kuzunguka mazabahu yako, Ee Yehova,
7 Ili nifanye sauti ya kutoa shukrani isikike+Na ili nitangaze kazi zako zote za ajabu.
8 Yehova, ninapenda nyumba kwenye unakaa,+Mahali kwenye utukufu wako unakaa.+
9 Usinifagilie mbali* pamoja na watenda-zambi+Wala kuondoa uzima wangu pamoja na watu wenye jeuri,*
10 Wenye mikono yao inajiingiza katika mwenendo wa haya,Na wenye mukono wao wa kuume umejaa rushwa.*
11 Lakini mimi, nitatembea katika uaminifu-mushikamanifu wangu.
Uniokoe* na unionyeshe wema.
12 Muguu wangu umesimama mahali tambarare;+Katika kutaniko kubwa,* nitamusifu Yehova.+
Maelezo ya Chini
^ Ao “hisia zangu za ndani kabisa.” Tnn., “figo zangu.”
^ Tnn., “Sikae.”
^ Ao “sichangamane na wanafiki.”
^ Tnn., “kukaa.”
^ Ao “Usifagilie mbali nafsi yangu.”
^ Ao “watu wenye kumwanga damu.”
^ Ao “kata-midomo.”
^ Tnn., “Unikomboe.”
^ Tnn., “Katika mikusanyiko.”