Zaburi 26:1-12

  • Kutembea katika uaminifu-mushikamanifu

    • “Unichunguze, Ee Yehova” (2)

    • Kuepuka mashirika ya mubaya (4, 5)

    • ‘Nitatembea kuzunguka mazabahu ya Mungu’ (6)

Ya Daudi. 26  Unihukumu, Ee Yehova, kwa maana nimetembea katika uaminifu-mushikamanifu wangu;+Nimemutegemea Yehova bila kuyumba-yumba.+  2  Unichunguze, Ee Yehova, na unijaribu;Usafishe mawazo yangu ya ndani kabisa* na pia moyo wangu.+  3  Kwa maana upendo wako mushikamanifu uko mbele yangu sikuzote,Na ninatembea katika kweli yako.+  4  Sishirikiane* na watu wadanganyifu,+Na ninaepuka wale wenye kuficha namna wako.*  5  Ninachukia kuwa pamoja na waovu,+Na ninakataa kushirikiana* na waovu.+  6  Nitanawa mikono yangu katika kukosa kuwa na hatia,Na nitatembea kuzunguka mazabahu yako, Ee Yehova,  7  Ili nifanye sauti ya kutoa shukrani isikike+Na ili nitangaze kazi zako zote za ajabu.  8  Yehova, ninapenda nyumba kwenye unakaa,+Mahali kwenye utukufu wako unakaa.+  9  Usinifagilie mbali* pamoja na watenda-zambi+Wala kuondoa uzima wangu pamoja na watu wenye jeuri,* 10  Wenye mikono yao inajiingiza katika mwenendo wa haya,Na wenye mukono wao wa kuume umejaa rushwa.* 11  Lakini mimi, nitatembea katika uaminifu-mushikamanifu wangu. Uniokoe* na unionyeshe wema. 12  Muguu wangu umesimama mahali tambarare;+Katika kutaniko kubwa,* nitamusifu Yehova.+

Maelezo ya Chini

Ao “hisia zangu za ndani kabisa.” Tnn., “figo zangu.”
Tnn., “Sikae.”
Ao “sichangamane na wanafiki.”
Tnn., “kukaa.”
Ao “Usifagilie mbali nafsi yangu.”
Ao “watu wenye kumwanga damu.”
Ao “kata-midomo.”
Tnn., “Unikomboe.”
Tnn., “Katika mikusanyiko.”