Zaburi 27:1-14
Ya Daudi.
27 Yehova ni mwangaza wangu+ na wokovu wangu.
Nimuogope nani?+
Yehova ni ngome ya uzima wangu.+
Nimuhofu nani?
2 Wakati waovu walinishambulia ili wameze mwili wangu,+Wapinzani wangu na maadui wangu ndio walijikwaa na kuanguka.
3 Hata kama jeshi linapiga kambi ili kunishambulia,Moyo wangu hautaogopa.+
Hata kama vita inaanza juu yangu,Bado nitaendelea kuwa hodari.
4 Nimemuomba Yehova jambo moja—Ni hilo nitatafuta—Kwamba nikae katika nyumba ya Yehova sikuzote za maisha yangu,+Ili kuangalia uzuri wa YehovaNa kuangalia kwa usamini* hekalu lake.*+
5 Kwa maana atanificha katika kibanda chake siku ya musiba;+Atanificha mahali pa siri katika hema yake;+Atanitia juu kwenye mwamba.+
6 Sasa kichwa changu kiko juu sana ya maadui wangu wenye kunizunguka;Nitatoa zabihu katika hema yake kwa makelele ya shangwe;Nitamuimbia Yehova sifa.*
7 Unisikie, Ee Yehova, wakati ninalia kwa sauti;+Unionyeshe wema na unijibu.+
8 Ukizungumuza kwa ajili yako, moyo wangu umesema:
“Tafuta uso wangu.”
Nitatafuta uso wako, Ee Yehova.+
9 Usinifiche uso wako.+
Usimufukuze mutumishi wako katika kasirani yako.
Wewe ni musaidizi wangu;+Usinitupe wala usiniache, Mungu wangu wa wokovu.
10 Hata kama baba yangu na mama yangu wananiacha,+Yehova mwenyewe atanikaribisha.+
11 Unifundishe njia yako, Ee Yehova,+Uniongoze katika pito la unyoofu kwa sababu ya maadui wangu.
12 Usinitie katika mukono wa maadui wangu,+Kwa maana mashahidi wa uongo wameinuka juu yangu,+Na wananiogopesha kupitia jeuri.
13 Ningekuwa wapi kama singekuwa na imaniKwamba nitaona wema wa Yehova katika inchi ya wazima?*+
14 Umutumainie Yehova;+Ukuwe hodari na moyo wako ukuwe na nguvu.+
Ndiyo, umutumainie Yehova.

