Zaburi 27:1-14

  • Yehova ni ngome ya uzima wangu

    • Kusamini hekalu la Mungu (4)

    • Yehova anamuhangaikia mutu hata kama wazazi hawamuhangaikie (10)

    • “Umutumainie Yehova” (14)

Ya Daudi. 27  Yehova ni mwangaza wangu+ na wokovu wangu. Nimuogope nani?+ Yehova ni ngome ya uzima wangu.+ Nimuhofu nani?   Wakati waovu walinishambulia ili wameze mwili wangu,+ Wapinzani wangu na maadui wangu ndio walijikwaa na kuanguka.   Hata kama jeshi linapiga kambi ili kunishambulia, Moyo wangu hautaogopa.+ Hata kama vita inaanza juu yangu, Bado nitaendelea kuwa hodari.   Nimemuomba Yehova jambo moja ⁠—​Ni hilo nitatafuta⁠— Kwamba nikae katika nyumba ya Yehova sikuzote za maisha yangu,+ Ili kuangalia uzuri wa Yehova Na kuangalia kwa usamini* hekalu lake.*+   Kwa maana atanificha katika kibanda chake siku ya musiba;+ Atanificha mahali pa siri katika hema yake;+ Atanitia juu kwenye mwamba.+   Sasa kichwa changu kiko juu sana ya maadui wangu wenye kunizunguka; Nitatoa zabihu katika hema yake kwa makelele ya shangwe; Nitamuimbia Yehova sifa.*   Unisikie, Ee Yehova, wakati ninalia kwa sauti;+ Unionyeshe wema na unijibu.+   Ukizungumuza kwa ajili yako, moyo wangu umesema: “Tafuta uso wangu.” Nitatafuta uso wako, Ee Yehova.+   Usinifiche uso wako.+ Usimufukuze mutumishi wako katika kasirani yako. Wewe ni musaidizi wangu;+ Usinitupe wala usiniache, Mungu wangu wa wokovu. 10  Hata kama baba yangu na mama yangu wananiacha,+ Yehova mwenyewe atanikaribisha.+ 11  Unifundishe njia yako, Ee Yehova,+ Uniongoze katika pito la unyoofu kwa sababu ya maadui wangu. 12  Usinitie katika mukono wa maadui wangu,+ Kwa maana mashahidi wa uongo wameinuka juu yangu,+ Na wananiogopesha kupitia jeuri. 13  Ningekuwa wapi kama singekuwa na imani Kwamba nitaona wema wa Yehova katika inchi ya wazima?*+ 14  Umutumainie Yehova;+ Ukuwe hodari na moyo wako ukuwe na nguvu.+ Ndiyo, umutumainie Yehova.

Maelezo ya Chini

Ao “kuangalia kwa kufikiri sana.”
Ao “patakatifu pake.”
Ao “Nitamupigia Yehova muziki.”
Ao pengine, “Hakika niko na imani kwamba nitaona wema wa Yehova katika inchi ya wazima.”