Zaburi 58:1-11

  • Kuko Mungu mwenye kuhukumu dunia

    • Sala ya kuomba waovu wapewe azabu (6-8)

Kwa kiongozi; imepatanishwa na “Usiharibu.” Ya Daudi. Miktamu.* 58  Je, munaweza kuzungumuza kuhusu haki wakati mumenyamaza?+ Je, munaweza kuhukumu kwa unyoofu, ninyi wana wa binadamu?+  2  Kuliko kufanya vile, munapanga ukosefu wa haki katika moyo wenu,+Na mikono yenu inaeneza jeuri katika inchi.+  3  Waovu wanajiendesha mubaya* tangu kuzaliwa;Wako kichwa-nguvu, waongo tangu wakati wanazaliwa.  4  Sumu yao ni kama sumu ya nyoka;+Wao ni viziwi kama nyoka-kobra mwenye anafunga sikio lake.  5  Hatasikiliza sauti ya watu wenye kuchezesha nyoka,Hata wafanye uchawi kwa ufundi namna gani.  6  Ee Mungu, vunja meno yao katika vinywa vyao! Vunja mataya* ya simba hawa,* Ee Yehova!  7  Acha waishe kama maji yenye kukauka. Acha Yeye akunje upinde wake na kuwaangusha kwa mishale yake.  8  Acha wakuwe kama konokono mwenye anayeyuka wakati anatembea;Kama mutoto mwenye alikufia katika tumbo la mwanamuke na mwenye haone jua hata kidogo.  9  Mbele vyungu vyenu vya kupikia havijapata moto wa kuni za muti wa mukwamba,Ataharibu umajimaji na tawi lenye kuwaka, kama kwa upepo wa zoruba.+ 10  Mwenye haki atashangilia kwa sababu ameona kisasi;+Miguu yake italowana damu ya waovu.+ 11  Kisha watu watasema: “Hakika kuko zawabu kwa ajili ya mwenye haki.+ Kwa kweli kuko Mungu mwenye anahukumu katika dunia.”+

Maelezo ya Chini

Ao “wamepotoka.”
Mataya ni mifupa ya kinywa yenye kubeba meno.
Ao “wana-simba hawa wenye manyoya ya murefu kwenye shingo.”