Zaburi 58:1-11
-
Kuko Mungu mwenye kuhukumu dunia
-
Sala ya kuomba waovu wapewe azabu (6-8)
-
Kwa kiongozi; imepatanishwa na “Usiharibu.” Ya Daudi. Miktamu.*
58 Je, munaweza kuzungumuza kuhusu haki wakati mumenyamaza?+
Je, munaweza kuhukumu kwa unyoofu, ninyi wana wa binadamu?+
2 Kuliko kufanya vile, munapanga ukosefu wa haki katika moyo wenu,+Na mikono yenu inaeneza jeuri katika inchi.+
3 Waovu wanajiendesha mubaya* tangu kuzaliwa;Wako kichwa-nguvu, waongo tangu wakati wanazaliwa.
4 Sumu yao ni kama sumu ya nyoka;+Wao ni viziwi kama nyoka-kobra mwenye anafunga sikio lake.
5 Hatasikiliza sauti ya watu wenye kuchezesha nyoka,Hata wafanye uchawi kwa ufundi namna gani.
6 Ee Mungu, vunja meno yao katika vinywa vyao!
Vunja mataya* ya simba hawa,* Ee Yehova!
7 Acha waishe kama maji yenye kukauka.
Acha Yeye akunje upinde wake na kuwaangusha kwa mishale yake.
8 Acha wakuwe kama konokono mwenye anayeyuka wakati anatembea;Kama mutoto mwenye alikufia katika tumbo la mwanamuke na mwenye haone jua hata kidogo.
9 Mbele vyungu vyenu vya kupikia havijapata moto wa kuni za muti wa mukwamba,Ataharibu umajimaji na tawi lenye kuwaka, kama kwa upepo wa zoruba.+
10 Mwenye haki atashangilia kwa sababu ameona kisasi;+Miguu yake italowana damu ya waovu.+
11 Kisha watu watasema: “Hakika kuko zawabu kwa ajili ya mwenye haki.+
Kwa kweli kuko Mungu mwenye anahukumu katika dunia.”+
Maelezo ya Chini
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “wamepotoka.”
^ Mataya ni mifupa ya kinywa yenye kubeba meno.
^ Ao “wana-simba hawa wenye manyoya ya murefu kwenye shingo.”