Zaburi 104:1-35

  • Kumusifu Mungu kwa sababu ya maajabu ya uumbaji

    • Dunia itadumu milele (5)

    • Divai na mukate kwa ajili ya mwanadamu mwenye anaweza kufa (15)

    • “Kazi zako ni nyingi sana!” (24)

    • ‘Wakati roho inaondolewa, wanakufa’ (29)

104  Acha nimusifu* Yehova.+ Ee Yehova Mungu wangu, uko mukubwa sana.+ Umevaa utukufu* na uzuri.+  2  Umefunikwa mwangaza+ kama nguo;Unatandika mbingu kama kitambaa cha hema.+  3  Anajenga nguzo za vyumba vyake vya juu katika maji yenye kuwa juu,*+Anafanya mawingu kuwa gari lake,+Akienda juu ya mabawa ya upepo.+  4  Anafanya malaika wake kuwa roho,Watumishi wake kuwa moto wenye kuteketeza.+  5  Ameweka dunia imara juu ya misingi yake;+Haitahamishwa kutoka mahali pake* milele na milele.+  6  Uliifunika kwa maji yenye kuenda chini sana kama kwa nguo.+ Maji yalisimama juu ya milima.  7  Kwa kemeo lako yalikimbia;+Kwa sauti ya mungurumo wako yalikimbia kwa woga mukubwa  8 ⁠ —​Milima ilipanda+ na mabonde yakashuka⁠—Mahali kwenye ulifanya kwa ajili yake.  9  Uliweka mupaka wenye hayapaswe kuvuka,+Ili yasifunike dunia tena hata siku moja. 10  Anatuma chemchemi katika mabonde;Kati ya milima zinatiririka. 11  Zinapatia maji wanyama wote wa pori;Punda wa pori wanakata kiu yao. 12  Juu yake ndege wa anga wanakaa;Wanaimba katikati ya majani mengi. 13  Anamwangilia milima maji ya vyumba vyake vya juu.+ Dunia inashiba matunda ya kazi zako.+ 14  Anaotesha majani kwa ajili ya ngombeNa mimea ili wanadamu waitumie,+Ili kukomalisha chakula juu ya udongo 15  Na divai yenye inafanya moyo wa mwanadamu ufurahi,+Mafuta yenye inafanya uso ungae,Na mukate wenye unategemeza moyo wa mwanadamu mwenye anaweza kufa.+ 16  Miti ya Yehova imeshiba,Mierezi ya Lebanoni yenye alipanda, 17  Kwenye ndege wanatengeneza chicha.* Makao ya korongo+ ni miti ya miberoshi. 18  Milima mirefu ni ya mbuzi wa milima;+Miamba ni kimbilio la wibari.+ 19  Amefanya mwezi ili uonyeshe nyakati zenye ziliwekwa;Jua linajua muzuri wakati wa kushuka.+ 20  Unaleta giza, na usiku unaingia,+Wakati wanyama wote wa pori wanazunguka-zunguka. 21  Wana-simba* wananguruma ili wapate mawindo yao+Na wanatafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.+ 22  Wakati jua linatokea,Wanarudia na kulala katika mapango yao. 23  Mwanadamu anaenda kwenye kazi yake,Na anafanya kazi kwa jasho mupaka mangaribi. 24  Kazi zako ni nyingi sana, Ee Yehova!+ Umezifanya zote kwa hekima.+ Dunia imejaa vitu vyenye umefanya. 25  Kuko bahari, kubwa sana na pana,Inajaa viumbe vyenye uzima vyenye havina hesabu, vidogo na vikubwa.+ 26  Mashua* zinasafiri kule,Na Leviatani,*+ mwenye uliumba ili achezee ndani yake. 27  Wote wanakungojea weweIli uwapatie chakula chao kwa wakati wake.+ 28  Wanakusanya kile unawapatia.+ Wakati unafungua mukono wako, wanashiba vitu vya muzuri.+ 29  Wakati unaficha uso wako, wanavurugika. Kama unaondoa roho yao, wanakufa na kurudia katika mavumbi.+ 30  Kama unatuma roho yako, wanaumbwa,+Na unafanya upya uso wa inchi. 31  Utukufu wa Yehova utadumu milele. Yehova atashangilia katika kazi zake.+ 32  Anaangalia dunia, na inatetemeka;Anagusa milima, na inatoa moshi.+ 33  Nitamuimbia Yehova+ maisha yangu yote;Nitamuimbia Mungu wangu sifa* wakati wote wenye nitakuwa muzima.+ 34  Mawazo yangu yamupendeze.* Nitashangilia katika Yehova. 35  Watenda-zambi wataisha katika dunia,Na waovu hawatakuwa tena.+ Acha nimusifu* Yehova. Mumusifu Yah!*

Maelezo ya Chini

Ao “heshima.”
Ao “nafsi yangu imusifu.”
Tnn., “katika maji.”
Ao “Haitatikisika.”
Ao “nyumba; viota.”
Ao “Wana-simba wenye manyoya ya murefu kwenye shingo.”
Ao “mashua za maji; bateaux.”
Ao “Nitamupigia Mungu wangu muziki.”
Ao pengine, “Acha kufikiri sana kwangu juu yake kupendeze.”
Ao “nafsi yangu imusifu.”
Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.