Zaburi 41:1-13
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
41 Mwenye furaha ni mutu yeyote mwenye anamuhangaikia mutu wa hali ya chini;+Yehova atamuokoa katika siku ya musiba.
2 Yehova atamuchunga na kulinda uzima wake.
Atatangazwa kuwa mwenye furaha katika dunia;+Hautamutia hata kidogo katika mukono wa maadui wake ili wamutendee vile wanapenda.*+
3 Yehova atamutegemeza kwenye kitanda chake cha ugonjwa;+Wakati wa ugonjwa wake utabadilisha kabisa kitanda chake.
4 Kwa maana nilisema: “Ee Yehova, unionyeshe wema.+
Uniponyeshe,*+ kwa maana nimekutendea zambi.”+
5 Lakini maadui wangu wanasema mambo maovu kunihusu:
“Atakufa wakati gani na jina lake lipotee?”
6 Kama mumoja wao anakuja kuniona, moyo wake unasema uongo.
Anakusanya jambo lenye kuumiza la kusema;Kisha anatoka inje na kulieneza kila mahali.
7 Wale wote wenye kunichukia wanaambiana kwa sauti ya chini-chini;Wanapanga kunifanyia jambo fulani la mubaya:
8 “Jambo lenye kuogopesha limemufikia;Kwa kuwa sasa iko* chini, hatasimama tena.”+
9 Hata mutu mwenye nilikuwa ninaishi naye kwa amani, mwenye nilitumainia,+Mwenye alikuwa anakula mukate wangu, ameinua kisigino chake ili kuniumiza.*+
10 Lakini wewe, Ee Yehova, unionyeshe wema na uniinue,Ili niwalipe.
11 Kwa njia hii nitajua kwamba unapendezwa na mimi:
Wakati adui yangu hataweza kupiga vigelegele vya ushindi juu yangu.+
12 Lakini mimi, unanitegemeza kwa sababu ya uaminifu-mushikamanifu wangu;+Utaniweka mbele yako milele.+
13 Yehova, Mungu wa Israeli, asifiweKwa umilele wote.*+
Amina na Amina.

