Zaburi 41:1-13

  • Sala kwenye kitanda cha ugonjwa

    • Mungu anategemeza wagonjwa (3)

    • Anasalitiwa na rafiki wa karibu (9)

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi. 41  Mwenye furaha ni mutu yeyote mwenye anamuhangaikia mutu wa hali ya chini;+ Yehova atamuokoa katika siku ya musiba.   Yehova atamuchunga na kulinda uzima wake. Atatangazwa kuwa mwenye furaha katika dunia;+ Hautamutia hata kidogo katika mukono wa maadui wake ili wamutendee vile wanapenda.*+   Yehova atamutegemeza kwenye kitanda chake cha ugonjwa;+ Wakati wa ugonjwa wake utabadilisha kabisa kitanda chake.   Kwa maana nilisema: “Ee Yehova, unionyeshe wema.+ Uniponyeshe,*+ kwa maana nimekutendea zambi.”+   Lakini maadui wangu wanasema mambo maovu kunihusu: “Atakufa wakati gani na jina lake lipotee?”   Kama mumoja wao anakuja kuniona, moyo wake unasema uongo. Anakusanya jambo lenye kuumiza la kusema; Kisha anatoka inje na kulieneza kila mahali.   Wale wote wenye kunichukia wanaambiana kwa sauti ya chini-chini; Wanapanga kunifanyia jambo fulani la mubaya:   “Jambo lenye kuogopesha limemufikia; Kwa kuwa sasa iko* chini, hatasimama tena.”+   Hata mutu mwenye nilikuwa ninaishi naye kwa amani, mwenye nilitumainia,+ Mwenye alikuwa anakula mukate wangu, ameinua kisigino chake ili kuniumiza.*+ 10  Lakini wewe, Ee Yehova, unionyeshe wema na uniinue, Ili niwalipe. 11  Kwa njia hii nitajua kwamba unapendezwa na mimi: Wakati adui yangu hataweza kupiga vigelegele vya ushindi juu yangu.+ 12  Lakini mimi, unanitegemeza kwa sababu ya uaminifu-mushikamanifu wangu;+ Utaniweka mbele yako milele.+ 13  Yehova, Mungu wa Israeli, asifiwe Kwa umilele wote.*+ Amina na Amina.

Maelezo ya Chini

Ao “katika tamaa ya maadui wake; ao katika nafsi ya maadui wake.” Angalia Maana ya Maneno.
Ao “Uponyeshe nafsi yangu.”
Ao “eko.”
Ao “amenigeukia.”
Ao “Tangu milele mupaka milele.”