Zaburi 41:1-13

  • Sala kwenye kitanda cha ugonjwa

    • Mungu anategemeza wagonjwa (3)

    • Anasalitiwa na rafiki wa karibu (9)

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi. 41  Mwenye furaha ni mutu yeyote mwenye anamuhangaikia mutu wa hali ya chini;+Yehova atamuokoa katika siku ya musiba.  2  Yehova atamuchunga na kulinda uzima wake. Atatangazwa kuwa mwenye furaha katika dunia;+Hautamutia hata kidogo katika mukono wa maadui wake ili wamutendee vile wanapenda.*+  3  Yehova atamutegemeza kwenye kitanda chake cha ugonjwa;+Wakati wa ugonjwa wake utabadilisha kabisa kitanda chake.  4  Kwa maana nilisema: “Ee Yehova, unionyeshe wema.+ Uniponyeshe,*+ kwa maana nimekutendea zambi.”+  5  Lakini maadui wangu wanasema mambo maovu kunihusu: “Atakufa wakati gani na jina lake lipotee?”  6  Kama mumoja wao anakuja kuniona, moyo wake unasema uongo. Anakusanya jambo lenye kuumiza la kusema;Kisha anatoka inje na kulieneza kila mahali.  7  Wale wote wenye kunichukia wanaambiana kwa sauti ya chini-chini;Wanapanga kunifanyia jambo fulani la mubaya:  8  “Jambo lenye kuogopesha limemufikia;Kwa kuwa sasa iko* chini, hatasimama tena.”+  9  Hata mutu mwenye nilikuwa ninaishi naye kwa amani, mwenye nilitumainia,+Mwenye alikuwa anakula mukate wangu, ameinua kisigino chake ili kuniumiza.*+ 10  Lakini wewe, Ee Yehova, unionyeshe wema na uniinue,Ili niwalipe. 11  Kwa njia hii nitajua kwamba unapendezwa na mimi: Wakati adui yangu hataweza kupiga vigelegele vya ushindi juu yangu.+ 12  Lakini mimi, unanitegemeza kwa sababu ya uaminifu-mushikamanifu wangu;+Utaniweka mbele yako milele.+ 13  Yehova, Mungu wa Israeli, asifiweKwa umilele wote.*+ Amina na Amina.

Maelezo ya Chini

Ao “katika tamaa ya maadui wake; ao katika nafsi ya maadui wake.” Angalia Maana ya Maneno.
Ao “Uponyeshe nafsi yangu.”
Ao “eko.”
Ao “amenigeukia.”
Ao “Tangu milele mupaka milele.”