Zaburi 41:1-13
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
41 Mwenye furaha ni mutu yeyote mwenye anamuhangaikia mutu wa hali ya chini;+
Yehova atamuokoa katika siku ya musiba.
2 Yehova atamuchunga na kulinda uzima wake.
Atatangazwa kuwa mwenye furaha katika dunia;+
Hautamutia hata kidogo katika mukono wa maadui wake ili wamutendee vile wanapenda.*+
3 Yehova atamutegemeza kwenye kitanda chake cha ugonjwa;+
Wakati wa ugonjwa wake utabadilisha kabisa kitanda chake.
4 Kwa maana nilisema: “Ee Yehova, unionyeshe wema.+
Uniponyeshe,*+ kwa maana nimekutendea zambi.”+
5 Lakini maadui wangu wanasema mambo maovu kunihusu:
“Atakufa wakati gani na jina lake lipotee?”
6 Kama mumoja wao anakuja kuniona, moyo wake unasema uongo.
Anakusanya jambo lenye kuumiza la kusema;
Kisha anatoka inje na kulieneza kila mahali.
7 Wale wote wenye kunichukia wanaambiana kwa sauti ya chini-chini;
Wanapanga kunifanyia jambo fulani la mubaya:
8 “Jambo lenye kuogopesha limemufikia;
Kwa kuwa sasa iko* chini, hatasimama tena.”+
9 Hata mutu mwenye nilikuwa ninaishi naye kwa amani, mwenye nilitumainia,+
Mwenye alikuwa anakula mukate wangu, ameinua kisigino chake ili kuniumiza.*+
10 Lakini wewe, Ee Yehova, unionyeshe wema na uniinue,
Ili niwalipe.
11 Kwa njia hii nitajua kwamba unapendezwa na mimi:
Wakati adui yangu hataweza kupiga vigelegele vya ushindi juu yangu.+
12 Lakini mimi, unanitegemeza kwa sababu ya uaminifu-mushikamanifu wangu;+
Utaniweka mbele yako milele.+
13 Yehova, Mungu wa Israeli, asifiwe
Kwa umilele wote.*+
Amina na Amina.
Maelezo ya Chini
^ Ao “katika tamaa ya maadui wake; ao katika nafsi ya maadui wake.” Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “Uponyeshe nafsi yangu.”
^ Ao “eko.”
^ Ao “amenigeukia.”
^ Ao “Tangu milele mupaka milele.”