Zaburi 145:1-21
Sifa ya Daudi.
א [Aleph]
145 Nitakutukuza, Ee Mungu wangu Mufalme,+Nitasifu jina lako milele na milele.+
ב [Beth]
2 Nitakusifu muchana wote;+Nitasifu jina lako milele na milele.+
ג [Gimel]
3 Yehova ni mukubwa na anastahili kusifiwa sana;+Ukubwa wake hauchunguzike.*+
ד [Daleth]
4 Kizazi kwa kizazi kitasifu kazi zako;Watasimulia kuhusu matendo yako yenye nguvu.+
ה [He]
5 Watasema kuhusu utukufu mukubwa wa ukubwa wako+Na mimi nitafikiri sana* juu ya kazi zako za ajabu.
ו [Waw]
6 Watasema kuhusu matendo yako yenye kuogopesha sana,*Na mimi nitatangaza ukubwa wako.
ז [Zayin]
7 Watachangamuka wakati watakumbuka wema wako mwingi,+Na watapiga vigelegele vya shangwe kwa sababu ya haki yako.+
ח [Heth]
8 Yehova ni mwenye huruma* na rehema,+Hakasirike haraka na ni mwenye upendo mwingi mushikamanifu.+
ט [Teth]
9 Yehova ni mwema kwa wote,+Na rehema yake inaonekana katika kazi zake zote.
י [Yod]
10 Kazi zako zote zitakutukuza, Ee Yehova,+Na washikamanifu wako watakusifu.+
כ [Kaph]
11 Watatangaza utukufu wa ufalme wako+Na kusema kuhusu nguvu zako,+
ל [Lamed]
12 Ili kujulisha wanadamu matendo yako yenye nguvu+Na utukufu mukubwa wa ufalme wako.+
מ [Mem]
13 Ufalme wako ni ufalme wa milele,Na mamlaka yako yanadumu katika vizazi vyote.+
ס [Samekh]
14 Yehova anategemeza wale wote wenye kuanguka+Na anasimamisha wale wote wenye kuinama chini.+
ע [Ayin]
15 Macho yote yanakuangalia yakiwa na tumaini;Unawapatia chakula chao kwa wakati wake.+
פ [Pe]
16 Unafungua mukono wakoNa kutimiza tamaa ya kila kitu chenye uzima.+
צ [Tsade]
17 Yehova ni mwenye haki katika njia zake zote+Na mushikamanifu katika mambo yote yenye anafanya.+
ק [Qoph]
18 Yehova iko karibu na wale wote wenye kumuitia,+Wote wenye kumuitia katika ukweli.*+
ר [Resh]
19 Anatimiza tamaa ya wale wenye kumuogopa;+Anasikia kilio chao cha kuomba musaada, na anawaokoa.+
ש [Shin]
20 Yehova analinda wale wote wenye kumupenda,+Lakini ataharibu waovu wote.+
ת [Taw]
21 Kinywa changu kitatangaza sifa ya Yehova;+Acha kila kiumbe chenye uzima kisifu* jina lake takatifu milele na milele.+

