Zaburi 145:1-21

  • Kumusifu Mungu, Mufalme mukubwa

    • ‘Nitatangaza ukubwa wa Mungu’ (6)

    • “Yehova ni mwema kwa wote” (9)

    • “Washikamanifu wako watakusifu” (10)

    • Ufalme wa Mungu ni wa milele (13)

    • Mukono wa Mungu unatosheleza wote (16)

Sifa ya Daudi. א [Aleph] 145  Nitakutukuza, Ee Mungu wangu Mufalme,+Nitasifu jina lako milele na milele.+ ב [Beth]  2  Nitakusifu muchana wote;+Nitasifu jina lako milele na milele.+ ג [Gimel]  3  Yehova ni mukubwa na anastahili kusifiwa sana;+Ukubwa wake hauchunguzike.*+ ד [Daleth]  4  Kizazi kwa kizazi kitasifu kazi zako;Watasimulia kuhusu matendo yako yenye nguvu.+ ה [He]  5  Watasema kuhusu utukufu mukubwa wa ukubwa wako+Na mimi nitafikiri sana* juu ya kazi zako za ajabu. ו [Waw]  6  Watasema kuhusu matendo yako yenye kuogopesha sana,*Na mimi nitatangaza ukubwa wako. ז [Zayin]  7  Watachangamuka wakati watakumbuka wema wako mwingi,+Na watapiga vigelegele vya shangwe kwa sababu ya haki yako.+ ח [Heth]  8  Yehova ni mwenye huruma* na rehema,+Hakasirike haraka na ni mwenye upendo mwingi mushikamanifu.+ ט [Teth]  9  Yehova ni mwema kwa wote,+Na rehema yake inaonekana katika kazi zake zote. י [Yod] 10  Kazi zako zote zitakutukuza, Ee Yehova,+Na washikamanifu wako watakusifu.+ כ [Kaph] 11  Watatangaza utukufu wa ufalme wako+Na kusema kuhusu nguvu zako,+ ל [Lamed] 12  Ili kujulisha wanadamu matendo yako yenye nguvu+Na utukufu mukubwa wa ufalme wako.+ מ [Mem] 13  Ufalme wako ni ufalme wa milele,Na mamlaka yako yanadumu katika vizazi vyote.+ ס [Samekh] 14  Yehova anategemeza wale wote wenye kuanguka+Na anasimamisha wale wote wenye kuinama chini.+ ע [Ayin] 15  Macho yote yanakuangalia yakiwa na tumaini;Unawapatia chakula chao kwa wakati wake.+ פ [Pe] 16  Unafungua mukono wakoNa kutimiza tamaa ya kila kitu chenye uzima.+ צ [Tsade] 17  Yehova ni mwenye haki katika njia zake zote+Na mushikamanifu katika mambo yote yenye anafanya.+ ק [Qoph] 18  Yehova iko karibu na wale wote wenye kumuitia,+Wote wenye kumuitia katika ukweli.*+ ר [Resh] 19  Anatimiza tamaa ya wale wenye kumuogopa;+Anasikia kilio chao cha kuomba musaada, na anawaokoa.+ ש [Shin] 20  Yehova analinda wale wote wenye kumupenda,+Lakini ataharibu waovu wote.+ ת [Taw] 21  Kinywa changu kitatangaza sifa ya Yehova;+Acha kila kiumbe chenye uzima kisifu* jina lake takatifu milele na milele.+

Maelezo ya Chini

Ao “hauwezi kueleweka.”
Ao “nitatafakari.”
Ao “nguvu zako.”
Ao “neema.”
Ao “kwa unyoofu.”
Tnn., “Miili yote isifu.”