Zaburi 132:1-18
Wimbo wa Safari za Kupanda.
132 Ee Yehova, umukumbuke DaudiNa mateso yake yote;+
2 Namna alimuapia Yehova,Namna alimuwekea naziri Mwenye Nguvu wa Yakobo:+
3 “Sitaingia katika hema yangu, katika nyumba yangu.+
Sitalala kwenye kiti changu, kwenye kitanda changu;
4 Sitaruhusu macho yangu yalale usingizi,Wala kope zangu zisinzie
5 Mupaka wakati nitapata mahali kwa ajili ya Yehova,Makao ya muzuri* kwa ajili ya Mwenye Nguvu wa Yakobo.”+
6 Angalia! Tulisikia habari hiyo katika Efrata;+Tuliipata katika mashamba ya pori.+
7 Acha tuingie katika makao yake;*+Acha tuiname kwenye kiti cha miguu yake.+
8 Simama, Ee Yehova, ili ukuje mahali pako pa kupumuzikia,+Wewe na Sanduku la nguvu zako.+
9 Makuhani wako wavae haki,Na washikamanifu wako wapige vigelegele vya shangwe.
10 Kwa ajili ya Daudi mutumishi wako,Usimukatae* mutiwa-mafuta wako.+
11 Yehova amemuapia Daudi;Hakika hatakosa kutimiza neno lake:
“Mumoja wa wazao wako,*Nitamutia kwenye kiti chako cha ufalme.+
12 Kama wana wako wanashika agano languNa vikumbusho vyangu vyenye ninawafundisha,+Wana wao piaWatakaa kwenye kiti chako cha ufalme milele.”+
13 Kwa maana Yehova amechagua Sayuni;+Ametamani ikuwe makao yake:+
14 “Hapa ndipo mahali pangu pa kupumuzikia milele;Nitakaa hapa,+ kwa maana hiyo ndiyo tamaa yangu.
15 Nitapabariki sana kwa vyakula;Nitashibisha maskini wake kwa mikate.+
16 Makuhani wake nitawavalisha wokovu,+Na washikamanifu wake watapiga vigelegele vya shangwe.+
17 Kule nitafanya nguvu za Daudi zikomae.*
Nimetayarisha taa kwa ajili ya mutiwa-mafuta wangu.+
18 Nitavalisha maadui wake haya,Lakini taji lenye kuwa kwenye kichwa chake litasitawi.”+

