Zaburi 132:1-18

  • Daudi anachaguliwa na pia Sayuni

    • “Usimukatae mutiwa-mafuta wako” (10)

    • Makuhani wa Sayuni wanavalishwa wokovu (16)

Wimbo wa Safari za Kupanda. 132  Ee Yehova, umukumbuke DaudiNa mateso yake yote;+  2  Namna alimuapia Yehova,Namna alimuwekea naziri Mwenye Nguvu wa Yakobo:+  3  “Sitaingia katika hema yangu, katika nyumba yangu.+ Sitalala kwenye kiti changu, kwenye kitanda changu;  4  Sitaruhusu macho yangu yalale usingizi,Wala kope zangu zisinzie  5  Mupaka wakati nitapata mahali kwa ajili ya Yehova,Makao ya muzuri* kwa ajili ya Mwenye Nguvu wa Yakobo.”+  6  Angalia! Tulisikia habari hiyo katika Efrata;+Tuliipata katika mashamba ya pori.+  7  Acha tuingie katika makao yake;*+Acha tuiname kwenye kiti cha miguu yake.+  8  Simama, Ee Yehova, ili ukuje mahali pako pa kupumuzikia,+Wewe na Sanduku la nguvu zako.+  9  Makuhani wako wavae haki,Na washikamanifu wako wapige vigelegele vya shangwe. 10  Kwa ajili ya Daudi mutumishi wako,Usimukatae* mutiwa-mafuta wako.+ 11  Yehova amemuapia Daudi;Hakika hatakosa kutimiza neno lake: “Mumoja wa wazao wako,*Nitamutia kwenye kiti chako cha ufalme.+ 12  Kama wana wako wanashika agano languNa vikumbusho vyangu vyenye ninawafundisha,+Wana wao piaWatakaa kwenye kiti chako cha ufalme milele.”+ 13  Kwa maana Yehova amechagua Sayuni;+Ametamani ikuwe makao yake:+ 14  “Hapa ndipo mahali pangu pa kupumuzikia milele;Nitakaa hapa,+ kwa maana hiyo ndiyo tamaa yangu. 15  Nitapabariki sana kwa vyakula;Nitashibisha maskini wake kwa mikate.+ 16  Makuhani wake nitawavalisha wokovu,+Na washikamanifu wake watapiga vigelegele vya shangwe.+ 17  Kule nitafanya nguvu za Daudi zikomae.* Nimetayarisha taa kwa ajili ya mutiwa-mafuta wangu.+ 18  Nitavalisha maadui wake haya,Lakini taji lenye kuwa kwenye kichwa chake litasitawi.”+

Maelezo ya Chini

Ao “Tabenakulo kubwa.”
Ao “tabenakulo yake kubwa.”
Tnn., “Usigeuzie nyuma uso wa.”
Tnn., “wa uzao wa tumbo lako la uzazi.”
Tnn., “pembe ya Daudi ikomae.”