Zaburi 107:1-43
107 Mumushukuru Yehova, kwa maana yeye ni mwema;+Upendo wake mushikamanifu unadumu milele.+
2 Acha wale wenye walikombolewa* na Yehova waseme jambo hilo,Wale wenye alikomboa katika mukono wa* mupinzani,+
3 Wale wenye alikusanya pamoja kutoka katika inchi mbalimbali,+Kutoka mashariki na kutoka mangaribi,*Kutoka kaskazini na kutoka kusini.+
4 Walitanga-tanga katika nyika, katika jangwa;Hawakupata njia ya kuenda katika muji kwenye wangeweza kuishi.
5 Walikuwa na njaa na kiu;Walizimia* kwa sababu ya kuchoka sana.
6 Waliendelea kumulilia Yehova katika taabu yao;+Aliwaokoa katika shida yao.+
7 Aliwafanya watembee katika njia yenye kufaa+Ili wafike katika muji kwenye wangeweza kuishi.+
8 Watu wamushukuru Yehova+ kwa sababu ya upendo wake mushikamanifuNa kwa sababu ya kazi zake za ajabu zenye anatendea wana wa binadamu.+
9 Kwa maana ametosheleza wenye kiu*Na kujaza wenye njaa* kwa vitu vya muzuri.+
10 Wamoja kati yao walikuwa wanaishi katika giza nzito sana,Wafungwa katika mateso na vyuma.
11 Kwa maana walikuwa wameasi neno la Mungu;Hawakuheshimia shauri la Mwenye Kuwa Juu Zaidi.+
12 Kwa hiyo alinyenyekeza mioyo yao kupitia taabu;+Walijikwaa, na hapakukuwa mutu yeyote wa kuwasaidia.
13 Walimuomba Yehova awasaidie katika taabu yao;Akawaokoa katika shida yao.
14 Aliwatosha katika giza nzito sana,Na kukata pingu zao.+
15 Watu wamushukuru Yehova kwa sababu ya upendo wake mushikamanifu+Na kwa sababu ya kazi zake za ajabu zenye anatendea wana wa binadamu.
16 Kwa maana amevunja milango ya shabaNa kukata mapingo* ya chuma.+
17 Walikuwa wapumbavu na waliteseka+Kwa sababu ya makosa yao na zambi zao.+
18 Walipoteza hamu ya kula* vyakula vyote;Walikaribia milango mikubwa ya kifo.
19 Walikuwa wanamuomba Yehova awasaidie katika taabu yao;Na alikuwa anawaokoa katika shida yao.
20 Alikuwa anatuma neno lake na kuwaponyesha+Na kuwaokoa katika mashimo yenye walikuwa wamenaswa ndani.
21 Watu wamushukuru Yehova kwa sababu ya upendo wake mushikamanifuNa kwa sababu ya kazi zake za ajabu zenye anatendea wana wa binadamu.
22 Acha watoe zabihu za shukrani+Na kutangaza kazi zake kwa vigelegele vya shangwe.
23 Wale wenye kusafiri kwa mashua* juu ya bahari,Wenye kufanya biashara yao juu ya maji mengi,+
24 Wameona kazi za YehovaNa kazi zake za ajabu katika mahali kwenye maji yenye kuenda chini sana;+
25 Namna zoruba yenye upepo mukali inainuka kwa neno lake,+Na kuinua mawimbi ya bahari.
26 Wanapanda juu mupaka kwenye anga;Wanashuka mupaka katika sehemu za chini kabisa.
Uhodari wao unayeyuka* kwa sababu ya musiba wenye kukaribia.
27 Wanayumba-yumba na kuenda huku na huku kama mulevi,Na ufundi wao wote unakuwa hauna mafaa yoyote.+
28 Kisha wanamulilia Yehova kwa sauti kubwa katika taabu yao,+Na anawaokoa katika shida yao.
29 Anatuliza zoruba yenye upepo mukali;Mawimbi ya bahari yananyamaza.+
30 Wanashangilia wakati yanatulia,Na anawaongoza mupaka kwenye bandari* yenye wanatamani.
31 Watu wamushukuru Yehova kwa sababu ya upendo wake mushikamanifuNa kwa sababu ya kazi zake za ajabu zenye anatendea wana wa binadamu.+
32 Acha wamutukuze katika kutaniko la watu,+Na acha wamusifu katika baraza la* wazee.
33 Anageuza mito kuwa jangwa,Na chemchemi za maji kuwa udongo wenye kukauka,+
34 Eneo lenye kuzaa kuwa eneo lenye chumvi ambalo limeachwa,+Kwa sababu ya uovu wa wale wenye kukaa ndani yake.
35 Anageuza jangwa kuwa viziwa vya maji vyenye matete,Na inchi kavu kuwa chemchemi za maji.+
36 Anafanya wenye njaa wakae kule,+Ili wajenge muji kwenye wanaweza kuishi.+
37 Wanapanda mbegu katika mashamba na kupanda mashamba ya mizabibu+Yenye kuzaa mazao mengi.+
38 Anawabariki na wanaongezeka sana;Haache ngombe wao wapunguke.+
39 Lakini tena wanakuwa kidogo na kunyenyekezwaKwa sababu ya ukandamizaji, musiba, na huzuni.
40 Anamwanga zarau juu ya watu wenye vyeoNa kuwafanya watange-tange kwenye hakuna njia katika maeneo yenye yameachwa.+
41 Lakini analinda* maskini ili wasikandamizwe+Na kufanya familia zao zikuwe nyingi sana kama kundi.
42 Watu wanyoofu wanaona jambo hilo na kushangilia;+Lakini watu wote wenye hawako wenye haki wanafunga vinywa vyao.+
43 Mutu yeyote mwenye kuwa na hekima atachunguza mambo hayo+Na atafikiria kwa uangalifu matendo ya Yehova ya upendo mushikamanifu.+
Maelezo ya Chini
^ Ao “walinunuliwa.”
^ Ao “nguvu za.”
^ Ao “Kutoka mahali jua linatokea na kutoka mahali jua linashukia.”
^ Ao “Nafsi yao ilizimia.”
^ Ao “nafsi yenye kukauka.”
^ Ao “nafsi yenye njaa.”
^ Pingo ni kipande cha muti ao cha chuma cha kufungia mulango kwa ndani.
^ Ao “Nafsi yao ilichukia kabisa.”
^ Ao “mashua za maji; bateaux.”
^ Ao “Nafsi yao inayeyuka.”
^ Bandari ni mahali mashua zinaegesha.
^ Tnn., “kiti cha.”
^ Ao “anainua juu,” ni kusema, ili wasifikiwe.