Zaburi 22:1-31
Kwa kiongozi; imepatanishwa na “Paa Dike wa Mapambazuko.”* Muziki wa Daudi.
22 Mungu wangu, Mungu wangu, sababu gani umeniacha?+
Sababu gani uko mbali usiweze kuniokoa,
Mbali na vilio vyangu vya uchungu?+
2 Mungu wangu, ninaendelea kuita wakati wa muchana, na wewe haunijibu;+
Na wakati wa usiku sinyamaze.
3 Lakini wewe ni mutakatifu,+
Umezungukwa na* sifa za Israeli.
4 Baba zetu walikutegemea wewe;+
Walitegemea, na ulikuwa unawaokoa.+
5 Walikulilia kwa sauti, na wakaokolewa;
Walikutegemea, na hawakufanywa wapoteze tumaini.*+
6 Lakini mimi ni munyoo na siko mwanadamu,
Ninachekwa* na wanadamu na kuzarauliwa na watu.+
7 Wale wote wenye wananiona wananichekelea;+
Wanazomea na kutikisa vichwa vyao kwa zarau:+
8 “Alijitia katika mikono ya Yehova. Acha Yeye amukomboe!
Acha Yeye amuokoe, kwa sababu Yeye anamupenda sana!”+
9 Wewe ndiye ulinitosha katika tumbo la uzazi,+
Ni Wewe ulinifanya nijisikie salama kwenye maziwa ya mama yangu.
10 Nimewekwa chini ya utunzaji wako* tangu kuzaliwa kwangu;
Tangu wakati nilikuwa katika tumbo la uzazi la mama yangu, umekuwa Mungu wangu.
11 Usibakie mbali na mimi, kwa maana taabu iko karibu+
Na sina musaidizi mwingine.+
12 Ngombe-dume wengi wadogo wananizunguka;+
Ngombe-dume wenye nguvu wa Bashani wananizunguka kwa ajili ya vita.+
13 Wanafungua vinywa vyao wazi juu yangu,+
Kama simba mwenye kunguruma mwenye anapasua mawindo yake vipande-vipande.+
14 Nimemwangwa kama maji;
Mifupa yangu yote imeteguka.
Moyo wangu umekuwa kama nta;*+
Unayeyuka katika sehemu zangu za ndani kabisa.+
15 Nguvu zangu zimekauka kama kipande cha chombo cha udongo;+
Ulimi wangu unashikamana na fizi* zangu;+
Unanishusha chini kwenye mavumbi ya kifo.+
16 Kwa maana imbwa wananizunguka;+
Wananizunguka kwa ajili ya vita kama kikundi cha watenda maovu,+
Kama vile simba, wako kwenye mikono yangu na miguu yangu.+
17 Ninaweza kuhesabu mifupa yangu yote.+
Wananiangalia na kunikazia macho.
18 Wanagawana nguo zangu kati yao wenyewe,
Na wanapigia nguo zangu kura.+
19 Lakini wewe, Ee Yehova, usiendelee kukaa mbali.+
Wewe ni nguvu zangu; kuja haraka unisaidie.+
20 Uniokoe* kutokana na upanga,
Uzima wangu wenye samani* kutokana na muguu wa* imbwa;+
21 Uniokoe kutoka katika kinywa cha simba+ na pembe za ngombe-dume wa pori;
Unijibu na uniokoe.
22 Nitatangaza jina lako kwa ndugu zangu;+
Katikati ya kutaniko nitakusifu.+
23 Ninyi wenye kumuogopa Yehova, mumusifu!
Ninyi wote uzao wa* Yakobo, mumutukuze!+
Mumuogope sana, ninyi wote uzao wa* Israeli.
24 Kwa maana hajazarau wala kuchukizwa na mateso ya ule mwenye kukandamizwa;+
Hajamuficha uso wake.+
Wakati alimulilia amusaidie, alisikia.+
25 Nitakusifu katika kutaniko kubwa;+
Nitatimiza naziri zangu mbele ya wale wenye kumuogopa.
26 Wapole watakula na kushiba;+
Wale wenye kumutafuta Yehova watamusifu.+
Mufurahie maisha* milele.
27 Miisho yote ya dunia itakumbuka na kumuendea Yehova.
Familia zote za mataifa zitainama mbele yako.+
28 Kwa maana ufalme ni wa Yehova;+
Anatawala juu ya mataifa.
29 Watu wote wenye kufanikiwa* katika dunia watakula na kumuinamia;
Wale wote wenye kushuka katika mavumbi watapiga magoti mbele yake;
Hakuna mutu yeyote kati yao mwenye anaweza kulinda uzima wao.*
30 Wazao wao watamutumikia;*
Kizazi chenye kitakuja kitaambiwa kuhusu Yehova.
31 Watakuja na kusimulia kuhusu haki yake.
Wataambia watu wenye bado hawajazaliwa mambo yenye amefanya.
Maelezo ya Chini
^ Pengine ni sauti ao mutindo wa muziki.
^ Ao “Umekaa ukiwa mufalme kati ya (juu ya).”
^ Ao “hawakupatishwa haya.”
^ Ao “Ninalaumiwa.”
^ Tnn., “Nimetupwa kwako.”
^ Inaonekana ni kitu chenye kutengenezwa na nyuki ili kuweka asali na chenye kinayeyuka haraka.
^ Fizi ni nyama zenye kushikilia meno katika kinywa.
^ Ao “Uokoe nafsi yangu.”
^ Tnn., “Kitu changu cha pekee,” ni kusema, nafsi yake, ao uzima wake.
^ Tnn., “mukono wa.”
^ Tnn., “mbegu ya.”
^ Tnn., “mbegu ya.”
^ Tnn., “Moyo wenu uishi.”
^ Tnn., “wanene.”
^ Ao “nafsi zao.”
^ Tnn., “Mbegu yao itamutumikia.”