Zaburi 103:1-22
Ya Daudi.
103 Acha nimusifu* Yehova;Acha kila kitu chenye kuwa ndani yangu kisifu jina lake takatifu.
2 Acha nimusifu* Yehova;Nisisahau hata kidogo mambo yote yenye amefanya.+
3 Anasamehe makosa yako yote+Na anaponyesha magonjwa yako yote;+
4 Anaokoa uzima wako kutoka katika shimo*+Na anakuvalisha taji la upendo wake mushikamanifu na rehema.+
5 Anakushibisha kwa vitu vya muzuri+ maisha yako yote,Na hivyo ujana wako unafanywa upya kama ule wa tai.+
6 Yehova anatenda kwa uadilifu*+ na hakiKwa ajili ya wote wenye kukandamizwa.+
7 Alimujulisha Musa njia zake,+Na wana wa Israeli matendo yake.+
8 Yehova ni mwenye rehema na huruma,*+Hakasirike haraka na ni mwenye upendo mwingi mushikamanifu.*+
9 Hatatafuta makosa sikuzote,+Wala hataendelea kuwa na kinyongo milele.+
10 Hajatutendea kulingana na zambi zetu,+Wala hajatulipa malipo yenye makosa yetu yanastahili.+
11 Kwa maana kama vile mbingu ziko juu kuliko dunia,Ni vile upendo wake mushikamanifu uko mwingi kuelekea wale wenye kumuogopa.+
12 Kama vile mahali jua linatokea kuko mbali sana na mahali jua linashukia,Ni vile ametia zambi zetu mbali sana na sisi.+
13 Kama vile baba anaonyesha wana wake rehema,Ni vile Yehova ameonyesha rehema wale wenye kumuogopa.+
14 Kwa maana anajua muzuri namna tumeumbwa,+Anakumbuka kwamba tuko mavumbi.+
15 Kuhusu mwanadamu mwenye anaweza kufa, siku zake ziko kama za majani;+Anachanuka kama ua la shamba.+
16 Lakini wakati upepo unavuma, haliko tena,Kama vile halijapata kuwa pale.*
17 Lakini upendo mushikamanifu wa Yehova ni wa umilele wote*Kuelekea wale wenye kumuogopa,+Na haki yake kuelekea watoto wa watoto wao,+
18 Kuelekea wale wenye kushika agano lake+Na wale wenye kuwa waangalifu ili kushika maagizo yake.
19 Yehova amefanya kiti chake cha ufalme kikuwe imara kabisa mbinguni;+Na ufalme wake unatawala juu ya kila kitu.+
20 Mumusifu Yehova, ninyi malaika wake wote,+ wenye nguvu nyingi sana,*Wenye kushika neno lake,+ kwa kutii sauti yake.*
21 Mumusifu Yehova, majeshi yake yote,+Watumishi wake wenye kufanya mapenzi yake.+
22 Mumusifu Yehova, kazi zake zote,Mahali pote penye anatawala.*
Nafsi yangu yote imusifu Yehova.
Maelezo ya Chini
^ Ao “nafsi yangu imusifu.”
^ Ao “nafsi yangu imusifu.”
^ Ao “kaburi.”
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “mwenye neema.”
^ Ao “fazili nyingi zenye upendo.”
^ Tnn., “Na mahali pake hapalijue tena.”
^ Ao “tangu milele mupaka milele.”
^ Ao “wenye uwezo katika nguvu.”
^ Tnn., “kwa kusikia sauti ya (mulio wa) neno lake.”
^ Ao “Mahali pote pa mamlaka yake makubwa zaidi.”