Zaburi 38:1-22
Muziki wa Daudi, wa kukumbusha.
38 Ee Yehova, usinikaripie katika hasira yako,Wala usinirekebishe katika kasirani yako kali.+
2 Kwa maana mishale yako imenitoboa ndani kabisa,Na mukono wako unanifinyia chini.+
3 Mwili wangu wote ni mugonjwa* kwa sababu ya kasirani yako kali.
Hakuna amani ndani ya mifupa yangu kwa sababu ya zambi yangu.+
4 Kwa maana makosa yangu yamekuwa mengi sana juu ya kichwa changu;+Kama muzigo muzito, ni mengi sana siwezi kuyabeba.
5 Vidonda vyangu vinanuka na viko na usahaKwa sababu ya upumbavu wangu.
6 Nimesumbuka na kushuka moyo sana;Ninatembea huku na huku muchana wote nikiwa na huzuni.
7 Kuko moto ndani ya mwili wangu;*Mwili wangu wote ni mugonjwa.+
8 Sihisi tena chochote na nimepondwa kabisa;Moyo wangu wenye uchungu mwingi unanifanya nilie kwa maumivu kwa sauti kubwa.*
9 Ee Yehova, tamaa zangu zote ziko mbele yako,Na kilio changu cha maumivu hakijafichwa mbele yako.
10 Moyo wangu unapiga-piga, nguvu zangu zimeisha,Na mwangaza wa macho yangu umeisha.+
11 Marafiki wangu na wenzangu wananiepuka kwa sababu ya pigo langu,Na marafiki wangu wa karibu wanasimama mbali.
12 Wale wenye kutafuta uzima wangu* wanatega mitego;Wale wenye kujaribu kunifanya mubaya wanazungumuza kuhusu kuniharibu;+Wanasema udanganyifu kwa sauti ya chini muchana wote.
13 Lakini kama kiziwi, sikukuwa ninawasikiliza;+Na kama bubu, sikukuwa ninafungua kinywa changu.+
14 Nimekuwa kama mutu mwenye hawezi kusikia,Mwenye kinywa chake hakina jambo lolote la kusema ili kujitetea.
15 Kwa maana nilikungojea wewe, Ee Yehova,+Na ukanijibu, Ee Yehova Mungu wangu.+
16 Kwa maana nilisema: “Acha wasishangilie juu ya magumu yanguWala kujiinua juu yangu kama muguu wangu unatereza.”
17 Kwa maana nilikuwa karibu kuanguka,Na maumivu yangu yalikuwa pamoja na mimi sikuzote.+
18 Niliungama kosa langu;+Nilisumbuliwa na zambi yangu.+
19 Lakini maadui wangu wako na nguvu* na wako na uwezo,*Wale wenye kunichukia bila sababu wamekuwa wengi sana.
20 Walinilipa ubaya kwa wema;Walikuwa wananipinga kwa sababu ya kufuatilia mambo mema.
21 Usiniache, Ee Yehova.
Ee Mungu, usiendelee kukaa mbali na mimi.+
22 Fanya haraka ili unisaidie,Ee Yehova, wokovu wangu.+
Maelezo ya Chini
^ Tnn., “Hakuna mahali popote pazima katika mwili wangu.”
^ Tnn., “Viuno vyangu vimejaa moto.”
^ Ao “ningurume.”
^ Ao “nafsi yangu.”
^ Tnn., “wako wazima.”
^ Ao pengine, “Lakini wale wenye ni maadui wangu bila sababu ni wengi.”