Zaburi 38:1-22

  • Sala ya mutu mwenye alitubu mwenye anateseka

    • “Nimesumbuka na kushuka moyo sana” (6)

    • Yehova anasikia wale wenye kumungojea (15)

    • “Nilisumbuliwa na zambi yangu” (18)

Muziki wa Daudi, wa kukumbusha. 38  Ee Yehova, usinikaripie katika hasira yako,Wala usinirekebishe katika kasirani yako kali.+  2  Kwa maana mishale yako imenitoboa ndani kabisa,Na mukono wako unanifinyia chini.+  3  Mwili wangu wote ni mugonjwa* kwa sababu ya kasirani yako kali. Hakuna amani ndani ya mifupa yangu kwa sababu ya zambi yangu.+  4  Kwa maana makosa yangu yamekuwa mengi sana juu ya kichwa changu;+Kama muzigo muzito, ni mengi sana siwezi kuyabeba.  5  Vidonda vyangu vinanuka na viko na usahaKwa sababu ya upumbavu wangu.  6  Nimesumbuka na kushuka moyo sana;Ninatembea huku na huku muchana wote nikiwa na huzuni.  7  Kuko moto ndani ya mwili wangu;*Mwili wangu wote ni mugonjwa.+  8  Sihisi tena chochote na nimepondwa kabisa;Moyo wangu wenye uchungu mwingi unanifanya nilie kwa maumivu kwa sauti kubwa.*  9  Ee Yehova, tamaa zangu zote ziko mbele yako,Na kilio changu cha maumivu hakijafichwa mbele yako. 10  Moyo wangu unapiga-piga, nguvu zangu zimeisha,Na mwangaza wa macho yangu umeisha.+ 11  Marafiki wangu na wenzangu wananiepuka kwa sababu ya pigo langu,Na marafiki wangu wa karibu wanasimama mbali. 12  Wale wenye kutafuta uzima wangu* wanatega mitego;Wale wenye kujaribu kunifanya mubaya wanazungumuza kuhusu kuniharibu;+Wanasema udanganyifu kwa sauti ya chini muchana wote. 13  Lakini kama kiziwi, sikukuwa ninawasikiliza;+Na kama bubu, sikukuwa ninafungua kinywa changu.+ 14  Nimekuwa kama mutu mwenye hawezi kusikia,Mwenye kinywa chake hakina jambo lolote la kusema ili kujitetea. 15  Kwa maana nilikungojea wewe, Ee Yehova,+Na ukanijibu, Ee Yehova Mungu wangu.+ 16  Kwa maana nilisema: “Acha wasishangilie juu ya magumu yanguWala kujiinua juu yangu kama muguu wangu unatereza.” 17  Kwa maana nilikuwa karibu kuanguka,Na maumivu yangu yalikuwa pamoja na mimi sikuzote.+ 18  Niliungama kosa langu;+Nilisumbuliwa na zambi yangu.+ 19  Lakini maadui wangu wako na nguvu* na wako na uwezo,*Wale wenye kunichukia bila sababu wamekuwa wengi sana. 20  Walinilipa ubaya kwa wema;Walikuwa wananipinga kwa sababu ya kufuatilia mambo mema. 21  Usiniache, Ee Yehova. Ee Mungu, usiendelee kukaa mbali na mimi.+ 22  Fanya haraka ili unisaidie,Ee Yehova, wokovu wangu.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “Hakuna mahali popote pazima katika mwili wangu.”
Tnn., “Viuno vyangu vimejaa moto.”
Ao “ningurume.”
Ao “nafsi yangu.”
Tnn., “wako wazima.”
Ao pengine, “Lakini wale wenye ni maadui wangu bila sababu ni wengi.”