Zaburi 38:1-22
Muziki wa Daudi, wa kukumbusha.
38 Ee Yehova, usinikaripie katika hasira yako,
Wala usinirekebishe katika kasirani yako kali.+
2 Kwa maana mishale yako imenitoboa ndani kabisa,
Na mukono wako unanifinyia chini.+
3 Mwili wangu wote ni mugonjwa* kwa sababu ya kasirani yako kali.
Hakuna amani ndani ya mifupa yangu kwa sababu ya zambi yangu.+
4 Kwa maana makosa yangu yamekuwa mengi sana juu ya kichwa changu;+
Kama muzigo muzito, ni mengi sana siwezi kuyabeba.
5 Vidonda vyangu vinanuka na viko na usaha
Kwa sababu ya upumbavu wangu.
6 Nimesumbuka na kushuka moyo sana;
Ninatembea huku na huku muchana wote nikiwa na huzuni.
7 Kuko moto ndani ya mwili wangu;*
Mwili wangu wote ni mugonjwa.+
8 Sihisi tena chochote na nimepondwa kabisa;
Moyo wangu wenye uchungu mwingi unanifanya nilie kwa maumivu kwa sauti kubwa.*
9 Ee Yehova, tamaa zangu zote ziko mbele yako,
Na kilio changu cha maumivu hakijafichwa mbele yako.
10 Moyo wangu unapiga-piga, nguvu zangu zimeisha,
Na mwangaza wa macho yangu umeisha.+
11 Marafiki wangu na wenzangu wananiepuka kwa sababu ya pigo langu,
Na marafiki wangu wa karibu wanasimama mbali.
12 Wale wenye kutafuta uzima wangu* wanatega mitego;
Wale wenye kujaribu kunifanya mubaya wanazungumuza kuhusu kuniharibu;+
Wanasema udanganyifu kwa sauti ya chini muchana wote.
13 Lakini kama kiziwi, sikukuwa ninawasikiliza;+
Na kama bubu, sikukuwa ninafungua kinywa changu.+
14 Nimekuwa kama mutu mwenye hawezi kusikia,
Mwenye kinywa chake hakina jambo lolote la kusema ili kujitetea.
15 Kwa maana nilikungojea wewe, Ee Yehova,+
Na ukanijibu, Ee Yehova Mungu wangu.+
16 Kwa maana nilisema: “Acha wasishangilie juu ya magumu yangu
Wala kujiinua juu yangu kama muguu wangu unatereza.”
17 Kwa maana nilikuwa karibu kuanguka,
Na maumivu yangu yalikuwa pamoja na mimi sikuzote.+
18 Niliungama kosa langu;+
Nilisumbuliwa na zambi yangu.+
19 Lakini maadui wangu wako na nguvu* na wako na uwezo,*
Wale wenye kunichukia bila sababu wamekuwa wengi sana.
20 Walinilipa ubaya kwa wema;
Walikuwa wananipinga kwa sababu ya kufuatilia mambo mema.
21 Usiniache, Ee Yehova.
Ee Mungu, usiendelee kukaa mbali na mimi.+
22 Fanya haraka ili unisaidie,
Ee Yehova, wokovu wangu.+
Maelezo ya Chini
^ Tnn., “Hakuna mahali popote pazima katika mwili wangu.”
^ Tnn., “Viuno vyangu vimejaa moto.”
^ Ao “ningurume.”
^ Ao “nafsi yangu.”
^ Tnn., “wako wazima.”
^ Ao pengine, “Lakini wale wenye ni maadui wangu bila sababu ni wengi.”