Zaburi 114:1-8

  • Israeli wanakombolewa kutoka Misri

    • Bahari ilikimbia (5)

    • Milima iliruka-ruka kama kondoo-dume (6)

    • Jiwe ngumu liligeuzwa kuwa chemchemi ya maji (8)

114  Wakati Israeli alitoka Misri,+Wakati nyumba ya Yakobo ilitoka kati ya watu wenye kuzungumuza luga ya kigeni,  2  Yuda ikakuwa patakatifu* pake,Israeli, eneo la utawala wake.+  3  Bahari iliona hilo na kukimbia;+Muto Yordani ulirudia nyuma.+  4  Milima iliruka-ruka kama kondoo-dume,+Vilima, kama wana-kondoo.  5  Ni nini ilikufanya ukimbie, Ee bahari?+ Sababu gani ulirudia nyuma, Ee Yordani?+  6  Sababu gani muliruka-ruka kama kondoo-dume, Enyi milima,Kama wana-kondoo, enyi vilima?  7  Tetemeka, Ee dunia, kwa sababu ya Bwana,Kwa sababu ya Mungu wa Yakobo,+  8  Mwenye anageuza mwamba kuwa kiziwa cha maji chenye matete,Jiwe ngumu kuwa chemchemi za maji.+

Maelezo ya Chini

Ao “mahali patakatifu.”