Zaburi 50:1-23

  • Mungu anahukumu kati ya mutu mushikamanifu na muovu

    • Agano pamoja na Mungu kupitia zabihu (5)

    • “Mungu mwenyewe ni Muamuzi” (6)

    • Wanyama wote ni wa Mungu (10, 11)

    • Mungu anafunua waovu (16-21)

Muziki wa Asafu.+ 50  Mungu wa miungu, Yehova,+ amesema;Anaita duniaKutoka mahali jua linatokea mupaka mahali linashukia.*  2  Kutoka Sayuni, ukamilifu wa uzuri,+ Mungu anaangaza.  3  Mungu wetu atakuja na hawezi kubakia kimya.+ Mbele yake kuko moto wenye kuteketeza,+Na zoruba kali inavuma kumuzunguka pande zote.+  4  Anaita mbingu zenye kuwa juu na dunia,+Ili ahukumu watu wake:+  5  “Munikusanyie washikamanifu wangu,Wale wenye kufanya agano pamoja na mimi kupitia zabihu.”+  6  Mbingu zinatangaza haki yake,Kwa maana Mungu mwenyewe ni Muamuzi.+ (Sela)  7  “Munisikilize, Enyi watu wangu, na mimi nitasema;Israeli, nitatoa ushahidi juu yako.+ Mimi ni Mungu, Mungu wako.+  8  Sikukaripie kwa sababu ya zabihu zako,Wala kwa sababu ya matoleo yako mazima ya kuteketezwa yenye kuwa mbele yangu kila wakati.+  9  Sihitaji kukamata ngombe-dume katika nyumba yako,Wala mbuzi* katika mazizi* yako.+ 10  Kwa maana kila munyama wa pori ni wangu,+Hata wanyama wenye kuwa juu ya milima elfu moja (1 000). 11  Ninajua kila ndege wa milima;+Wanyama wa pori wenye hawana hesabu ni wangu. 12  Kama ningekuwa na njaa, singekuambia,Kwa maana inchi yenye kuzaa na kila kitu chenye kuwa ndani ni changu.+ 13  Je, nitakula nyama ya ngombe-dumeNa kunywa damu ya mbuzi?+ 14  Toa shukrani zikiwa zabihu yako kwa Mungu,+Na utimize naziri zako kwa Mwenye Kuwa Juu Zaidi;+ 15  Uniitie wakati wa taabu.+ Nitakuokoa, na wewe utanitukuza.”+ 16  Lakini Mungu atamuambia muovu: “Uko na haki gani ya kueleza masharti yangu+Ao kuongea kuhusu agano langu?+ 17  Kwa maana unachukia nizamu,*Na unaendelea kugeuzia mugongo maneno yangu.*+ 18  Wakati unamuona mwizi, unapendezwa naye,*+Na unashirikiana na wazinifu. 19  Unatumia kinywa chako kueneza mambo ya mubaya,Na udanganyifu umeshikamana na ulimi wako.+ 20  Unakaa na kumusema mubaya ndugu yako mwenyewe;+Unafunua makosa ya* mwana wa mama yako mwenyewe. 21  Wakati ulifanya mambo hayo, nilibakia kimya,Kwa hiyo ukafikiri kwamba nitakuwa tu kama wewe. Lakini sasa nitakukaripia,Na nitakushitaki.+ 22  Tafazali, mufikirie jambo hili, ninyi wenye kumusahau Mungu,+Ili nisiwapasue vipande-vipande bila mutu wa kuwaokoa. 23  Ule mwenye anatoa shukrani kuwa zabihu yake ananitukuza,+Na kuhusu ule mwenye anafuata njia yenye iliwekwa,Nitamufanya aone wokovu wa Mungu.”+

Maelezo ya Chini

Ao “Kuanzia mashariki mupaka mangaribi.”
Tnn., “mbuzi-dume.”
Zizi ni lupango ya kuchungia wanyama.
Tnn., “kutupa maneno yangu nyuma yako.”
Ao “agizo.”
Ao pengine, “unajiunga naye.”
Ao “Unamuharibishia sifa.”