Zaburi 50:1-23
Muziki wa Asafu.+
50 Mungu wa miungu, Yehova,+ amesema;Anaita duniaKutoka mahali jua linatokea mupaka mahali linashukia.*
2 Kutoka Sayuni, ukamilifu wa uzuri,+ Mungu anaangaza.
3 Mungu wetu atakuja na hawezi kubakia kimya.+
Mbele yake kuko moto wenye kuteketeza,+Na zoruba kali inavuma kumuzunguka pande zote.+
4 Anaita mbingu zenye kuwa juu na dunia,+Ili ahukumu watu wake:+
5 “Munikusanyie washikamanifu wangu,Wale wenye kufanya agano pamoja na mimi kupitia zabihu.”+
6 Mbingu zinatangaza haki yake,Kwa maana Mungu mwenyewe ni Muamuzi.+ (Sela)
7 “Munisikilize, Enyi watu wangu, na mimi nitasema;Israeli, nitatoa ushahidi juu yako.+
Mimi ni Mungu, Mungu wako.+
8 Sikukaripie kwa sababu ya zabihu zako,Wala kwa sababu ya matoleo yako mazima ya kuteketezwa yenye kuwa mbele yangu kila wakati.+
9 Sihitaji kukamata ngombe-dume katika nyumba yako,Wala mbuzi* katika mazizi* yako.+
10 Kwa maana kila munyama wa pori ni wangu,+Hata wanyama wenye kuwa juu ya milima elfu moja (1 000).
11 Ninajua kila ndege wa milima;+Wanyama wa pori wenye hawana hesabu ni wangu.
12 Kama ningekuwa na njaa, singekuambia,Kwa maana inchi yenye kuzaa na kila kitu chenye kuwa ndani ni changu.+
13 Je, nitakula nyama ya ngombe-dumeNa kunywa damu ya mbuzi?+
14 Toa shukrani zikiwa zabihu yako kwa Mungu,+Na utimize naziri zako kwa Mwenye Kuwa Juu Zaidi;+
15 Uniitie wakati wa taabu.+
Nitakuokoa, na wewe utanitukuza.”+
16 Lakini Mungu atamuambia muovu:
“Uko na haki gani ya kueleza masharti yangu+Ao kuongea kuhusu agano langu?+
17 Kwa maana unachukia nizamu,*Na unaendelea kugeuzia mugongo maneno yangu.*+
18 Wakati unamuona mwizi, unapendezwa naye,*+Na unashirikiana na wazinifu.
19 Unatumia kinywa chako kueneza mambo ya mubaya,Na udanganyifu umeshikamana na ulimi wako.+
20 Unakaa na kumusema mubaya ndugu yako mwenyewe;+Unafunua makosa ya* mwana wa mama yako mwenyewe.
21 Wakati ulifanya mambo hayo, nilibakia kimya,Kwa hiyo ukafikiri kwamba nitakuwa tu kama wewe.
Lakini sasa nitakukaripia,Na nitakushitaki.+
22 Tafazali, mufikirie jambo hili, ninyi wenye kumusahau Mungu,+Ili nisiwapasue vipande-vipande bila mutu wa kuwaokoa.
23 Ule mwenye anatoa shukrani kuwa zabihu yake ananitukuza,+Na kuhusu ule mwenye anafuata njia yenye iliwekwa,Nitamufanya aone wokovu wa Mungu.”+

